
Tupac Shakur alimwambia msanii Madonna kwamba alivunja uhusiano wao wa
kimapenzi kutokana na rangi ya ngozi yake katika barua iliojawa na hisia
kwa msanii huyo wa muziki wa rap.
Barua hiyo ya 1995 ilioandikwa kwa ''M'' ilisema kuwa na mwanamume
mweusi kungeweza kumsaidia kikazi lakini hatua hiyo itawaudhi mashabiki
wake.
Madonna alithibitisha miaka miwili iliopita kwamba alikuwa na uhusiano
na Tupac Shakur ijapokuwa haijulikani ulichukua muda gani.
Barua hiyo inapigwa mnada huku bei yake ya kwanza ikiwa $ 100,000, Ikiwa
imeandikwa tarehe 15 mwezi Januari 1995, iliandikwa wakati Tupac
alipokuwa akihudumia kifungo jela kwa unyanyasaji wa kingono na ilijiri
miezi 18 kabla ya yeye kuuawa kwa kupigwa risasi.
Wasanii wote wawili walikuwa na umaarufu mkubwa na ''Kwa wewe kuonekana
na mtu mweusi hakungedhuru kazi yako kivyovyote na badala yake
kungefanya uonekana mtu uliye wazi na wa kufurahisha, Tupac aliyekuwa na
umri wa miaka 23 alimwandikia Madonna akiwa katika Jela ya New York
Clinton.
''Lakini kwangu mimi nilihisi kana kwamba kulingana na vile watu
wanavyonichukulia ningewaudhi nusu ya watu walionifanya kuwa
nilivyo',aliandika Madonna
''Kama ulivyosema, sijakuwa rafiki ambaye najua naweza kuwa'', aliandika Tupac , akiongezea, ''sikupenda kukuumiza moyo''.
Jarida la Rolling Stone lilithibitisha uhasilia wa barua hiyo ambayo ilichapishwa kwa mara ya kwanza na mtandao wa TMZ.
Tupac ambaye wazazi wake wote walikuwa wanaharakati wa Black Panther pia
alisema kwamba Madonna wakati huo akiwa na umri wa miaka 36 alimuumiza
moyo wakati aliposema katika mahojiano kwamba ''alikuwa amekwenda
kuwabadili tabia wachezaji wote wa mpira wa kikapu pamoja na wasanii
wote wa muziki wa rap''.
''Maneno hayo yaliniumiza moyo kwa sababu singedhani kwamba ulikuwa na
uhisano mwengine na msanii yeyote wa rap isipokuwa mimi'', aliandika
Tupac.
''Ni wakati huu ambapo baada ya kuumizwa moyo niliamua kujitetea na ndiposa nikasema mambo mengi''.
Aliongezea: tafadhali nielewe msimamo wangu wa awali kama kijana mdogo asiye na uzoefu.
Tupac alimalizia: Inafurahisha lakini uzoefu wangu umenifunza kutochukulia vitu vilivyo.
Mnamo mwezi Septemba tarehe 7 1996, msanii huyo ambaye aliuza rakodi
milioni 75 duniani alifariki katika mfyatuliano wa risasi akiwa katika
gari katika mji wa Las Vegas muda mfupi baada ya kutazama ndondi ambapo
Mike Tyson alikuwa akizipiga.
Barua hiyo itapigwa mnada katika eneo la Gotta Have Rock and Roll Sale,
ambao unatarajiwa kufanywa kati ya tarehe 18 na 19 mnamo mwezi Julai.