Jumamosi, 8 Julai 2017

Taifa Stars wamepata nafasi ya mshindi wa tatu vs Lesotho



 
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars jana July 7 2017 imefanikiwa kuingia kwenye headlines baada ya kupata ushindi katika game ya michuano ya COSAFA ya kutafuta mshindi wa tatu iliyochezwa Afrika Kusini. Taifa Stars game ya kutafuta mshindi wa tatu imecheza dhidi ya timu ya taifa ya Lesotho na dakika 90 zikamaliza kwa sare tasa (0-0) kutokana na timu hizo kutoshana nguvu na kila moja kufanikiwa kumiliki mpira kwa asilimia 50 ndio mikwaju ya penati ikaamua mshindi.




Licha ya Lesotho kuonekana kuwa wazuri kiasi na kufika golini kwa Taifa Stars mara nyingi lakinihawakuwa wazuri katika upigaji penati na wakajikuta wakifungwa kwa penati 4-2, huku kwa upande wa Tanzania Shiza Kichuya ndio alikosa penati, Himid Maoa, Simon Msuva, Abdi Banda na Raphael Alpha wakafunga penati zote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni