mwana wa liganga blog ni blog ya kutoa taarifa, matukio, yaliyotokea katika ulimwengu hususani katika nchi yaTanzania
blog hii inasimamiwa na mwandishi wa habari kitaaluma bwana Deus Thomas liganga.lengo ni kutoa taarifa kwa umma,kwa maendeleo ya taifa na Dunia kwa ujumla
kwa mawasiliano kuhusu mtangazo, habari, wasiliana nasi 0659944423,deusliganga@yahoo.com,mzeeliganga@gmail.com
watumishi wa mahakama mkoani morogoro wametakiwa kujifunza matumizi ya kompyuta ili kurahisisha kazi za muhimili huo, nakuingia katika mfumo wa tehama.
hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa morogoro Dk Steven Kebwe katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria ngazi ya mkoa , iliyofanyika manispaa y morogoro.
dk kebwe ambaye alikuwa mgeni rasmi alionya watumishi wa mahakama kuachana na vitendo vya rushwa ili kutoa haki kwa raia. sambasamba na raia kutojichukulia sheria mikononi .
Ni siku chache zimepita toka msanii Diamond Platnumz kudaiwa kutoka kimapenzi na wasichana wengine tofauti na mama watoto wake Zari the bosslady. Inasemekana kuwa Diamond Platnumz hupeleka wasichana tofautitofauti nyumbani kwake Madale, kutokana na tetesi zilizokuwa zikiendelea kwenye mitandao ya kijamii ikaonekana Zarikukasirishwa na tabia hiyo. Hivyo kupitia instagram account ya Zari ameonekana kumu’unfollow baba watoto wake Diamond Platnumz, kitu hiki kimeleta maswali mengi kwa baadhi ya mashabiki na wengi kuhusisha ukaribu uliotokea kati ya Wema Sepetuna Diamond siku ya uzinduzi wa kutambulisha rasmi Marombosso WCB.
February 1, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo amemteua Dkt. Adelardus Kilangikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Pia President JPM amemteua Paul Joel Ngwembe kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali (DAG) kuanzia February 1, 2018.
Balozi John Kijazi akitangaza uteuzi huu
mpya na nafasi walizopangiwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu George Masaju na
Naibu wake Gerson Mdemu.
Kampuni ya Mawasiliano Tanzania ya (TTCL), imefutwa na kubadilishwa kuwa Shirika (TTCL Corporation).
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam katika makao
makuu ya shirika hilo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Makame Mbarawa,
amesema kuwa anamshukuru sana Rais Magufuli kwa kuona umuhimu wa kuona
wa kuwa na shirika la mawasiliano madhubuti kwa ajili ya kuleta maslahi
mapana ya nchi, huku akitoa shukrani pia kwa Wabunge wote kwa kukubali
kupitisha muswada huo.
Aidha Prof Mbarawa, amesema uwepo wa sheria ya shirika la mawasiliano
unatoa fursa ya kuboresha sekta kwa kuweka mazingira mazuri ya usimamizi
wa miundombinu ya mikakati chini ya shirika hilo.
Profesa Mbarawa pia amewajulisha Watanzania wote kuwa mabadiliko ya
kuhama kutoka kampuni kuwa shirika la mawasiliano hayatawaathiri kwa
namna ya utoaji wa huduma mbalimbali ambazo zilikuwa zinatolewa na
kampuni ya simu ya (TTCL) huku akielezwa kuwa wanaodaiwa na iliyokuwa
kampuni hiyo watatakiwa kulia madeni yao kama mikataba yao inavyosema na
wanaoidai watalipwa pia.
Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi amesema pamoja na Simba kuendelea
kuongoza lakini bado wana kazi ngumu kutokana na ushindani wa ligi
ulivyo.
Simba inaongoza Ligi Kuu Bara kwa tofauti ya pointi tano tofauti ya Azam FC wanaoshika nafasi ya pili.
Okwi amesema wanaamini wako katika nafasi nzuri lakini lazima wafanye juhudi zaidi.
“Tunaongoza ligi kwa sasa, lakini utaona tofauti ni ndogo sana na
anayetufuatia. Maana yake kama timu tunatakiwa kuendelea kupambana hadi
mwisho.
“Ushindani ni mkali sana, kila timu inataka kufanya vizuri na sisi
tunataka kufanya vizuri. Tumekuwa tukijituma kama timu kwa faida ya
klabu yetu na tunajua bado tunatakiwa kujituma,” alisema.
Okwi ndiye anayeongoza kwa ufungaji wa mabao katika Ligi Kuu Bara akiwa na 12.
Mara nyingi anapohojiwa Okwi amesema kitu cha kwanza kwake ni timu kwa
kuwa kama mchezaji yeye na wenzake wamekuwa wakipigana kwa ajili ya
timu.
Rais John Magufuli leo February 1, 2018
katika Maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Mahakama amesema yupo tayari kufanya
uteuzi wa majaji wengine ili kukabiliana na changamoto ya upungufu
mkubwa wa majaji ambayo inasababisha mrundikano wa mashauri katika
Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani.
Tofauti na hilo Rais Magufuli ametoa wito kwa Mahakama kuendelea
kurekebisha dosari ambazo zimekuwa zikiuchafua mhimili huo wa Dola
ikiwemo Majaji na Mahakimu kujihusisha na vitendo vya upokeaji wa rushwa
na ucheleweshaji wa kesi ambavyo vinasababisha hasara kubwa kwa taifa.
Aidha amempongeza Jaji Mkuu Prof Ibrahim Juma kwa hatua ya kuwafukuza
kazi watumishi 112 wa Mahakama wakiwemo Mahakimu 17 waliojihusisha na
vitendo vya ukiukwaji wa maadili
Rais Magufuli pia ameeleza kushangazwa na vyombo vingine ambavyo
hushirikiana na Mahakama kama vile Jeshi la Polisi, Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Magereza na Ofisi ya Mkurugenzi wa
Mashitaka (DPP) kwa kutowawajibisha watumishi wake wanaokiuka maadili. “Mwaka jana nililalamika, sasa
mwaka huu sitalalamika, nitachukua hatua, tena mwezi huu wa pili
hautaisha, pale ofisini kwangu napokea barua nyingi za malalamiko ya
ucheleweshaji wa kesi, kila kesi upelelezi haujakamilika, ni lazima kuwe
na utatuzi wa jambo hili” – Rais Magufuli “Hivi sasa kuna kesi za
Shilingi Bilioni 169.1 na Dola za Marekani Milioni 38.2 zinasubiri tu na
nchi inakosa mapato” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.” – Rais Magufuli
Mwanaharakati
nchini Kenya Okiya Omtatah amefungua mashtaka dhidi ya serikali katika
Mahakama Kuu kutokana na uamuzi wake wa kuzima vituo vya
televisheni vya Citizen TV, NTV na KTN pamoja na Inooro TV siku ya ‘kujiapisha’ Kiongozi wa Upinzania NASA Raila Odinga. Omtatah ameeleza kuwa kufungiwa
kwa vyombo hivyo vya habari ni kinyume cha sheria na hakuna sheria
yoyote iliyowapa mamlaka ya kutekeleza suala hilo. Amedai kuwa serikali
hiyo lazima izuiwe katika kudharau utawala wa sheria jambo ambalo ni
msingi mkuu wa thamani ya taifa na kanuni ya utawala. Ameongeza kuwa anahitaji mahakama
iamuru serikali ilipe fidia vyombo hivyo vya habari vilivyofungwa na
kusababishiwa hasara kutokana na jambo hilo.
Dodoma. Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeliomba
Bunge kumuomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)
kufanya ukaguzi wa mchakato wa mikataba yote ya mradi wa Mlimani City.
Akiwasilisha bungeni leo Februari1, 2018 taarifa ya utekelezaji wa
shughuli za kamati hiyo mwenyekiti wa PAC, Naghenjwa Kaboyoka amesema
kamati hiyo imebaini dosari katika mkataba wa uendeshaji wa mradi huo,
kusababisha Serikali kukosa mapato.
Miongoni mwa dosari alizozitaja za mradi huo ni kukiukwa kwa sheria ya
Kituo Cha Uwekezaji Tanzania (TIC) inayotaka ili kibali cha uwekezaji
kutolewa lazima mwekezaji alete ushahidi kuwa na mtaji wa kutosha.
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kilikodisha eneo hilo kwa kampuni ya Mlimani Holding Ltd.
Hivi karibuni PAC ilifanya ziara katika eneo la Mlimani City na kuutaka
uongozi wa UDSM kurekebisha mkataba kati yake na kampuni ya Mlimani City
Holding Ltd kutokana na mapungufu yaliyojitokeza, huku ikihoji sababu
ya mwekezaji huyo kuja na mtaji wa Sh150,000 tu.
Licha ya kutotaja siku, Kaboyoka amesema mara ukaguzi huo utakapokamilika taarifa yake iwasilishwe bungeni.
Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na Serikali ya
Tanzania kupitia Wizara ya Kilimo wamesaini mkataba wa ushirikiano wenye
lengo la kuisaidia Tanzania kujenga uwezo wa kufuatilia na kudhibiti
uvamizi wa viwavi jeshi hapa nchini.
Akizungumza katika hafla ya makubaliano hayo mkoani Dodoma, Katibu Mkuu
wa Wizara ya Kilimo,Mhandisi Mathew Mtigumwe, amesema makubaliano hayo
yamekuja kwa wakati muafaka ambapo Serikali ilikuwa inachukua hatua
mbali mbali kukabiliana na tatizo hilo.
Mwakilishi Mkazi wa FAO,Fred Kafeero,amesema Shirika hilo limekuwa
likifanya kazi pamoja na Serikali katika nchi za Kusini mwa Afrika
ikiwemo Tanzania kudhibiti athari inayosababishwa na viwavi jeshi hivyo.
Kupitia makubaliano hayo,FAO itatoa msaada wa kiutaalamu na kifedha
wenye thamani ya Dola za Kimarekani 250,000 ambazo ni zaidi ya Tshs.
Milioni 550 kuimarisha ufuatiliaji na kukuza uelewa kuhusu viwavi jeshi
kwa mazao kabla na wakati wa misimu ya kilimo ijayo.
Muimbaji kutokea kwenye kundi la Good Lyfe Moses Sekibooga ambaye wengi wanamfahamu Radio kutokea Uganda imeripotiwa amefariki dunia asubuhi ya leo February 1,2018 baada ya kukaa ICU kwa siku kadhaa zilizopita, hii ni baada kuripotiwa kupata ajali ya gari January 23,2018.
Msanii huyo ambaye alikuwa akifanya vizuri na mwenzie Weasel, tangu
January 23 mwaka huu hali yake ilikuwa ikiripotiwa kuwa mbaya kufuatia
majereha aliyoyapata kutokana na ugomvi wa klabu.
Hapo jana Rais wa Uganda, Yoweri Museven alitoa Milioni 30 kwa ajili
ya matibabu ya msanii huyo, pia kulikuwa na maombi maalumu yalikuwa
yameandaliwa kwa ajili ya kumuombea ambayo yalitarajiwa kufanyika
February 4 mwaka huu katika kanisa la Light the World.
Radio
Muimbaji Radio ameacha pengo kubwa katika kundi la Good Lyfe ambalo liliundwa na yeye mwenyewe pamoja na Weasel ambaye ni mdogo wa muimbaji na legend wa muziki nchini Uganda Joseph Mayanja ambao wengi tunamfahamu kama Jose Chameleon.
Kutoka kushoto ni marehemu Radio akiwa na mwenzake Weasel
Taarifa za kifo cha Radio zinakuja ikiwa ni siku moja imepita toka Rais wa UgandaYoweri Musevenikuripotiwa kutoa milioni 30 kama mchango kwa ajili ya kuokoa maisha ya staa huyo kwa kugharamia matibabu. Radio na Weasel wamefanya nyimbo nyingi ambazo zimewahi pia kupata Air time katika TV na Radio Stations za Tanzania, Don’t Cry ft Wizkid, Zuena na wimbo wa Where You Are waliokuwa wameshirikishwa na Blu 3 na huu uliwafanya wajulikane zaidi Tanzania kutokana na wimbo huo kufanya vizuri.
Dar es Salaam. Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetoa mpangilio
wa ubora wa ufaulu kimikoa wa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2017, huku
Dar es Salaam ukikosekana katika mikoa 10 iliyofanya vizuri.
Hata hivyo, mkoa huo umepanda kutoka nafasi ya 18 mwaka juzi, hadi
nafasi ya 16 mwaka jana. Katika orodha hiyo mkoa wa Kilimanjaro umepanda
kutoka nafasi ya tano mwaka 2016 hadi nafasi ya kwanza mwaka jana.
Mkoa wa Pwani nao umepanda kutoka nafasi ya saba mwaka juzi hadi nafasi
ya pili mwaka jana. Katika orodha hiyo Tabora imeshika nafasi ya tatu
kutoka nafasi ya 10 mwaka 2016.
Mikoa mingine iliyofuata na nafasi iliyoshika ni Shinyanga (nafasi ya
nne kutoka nafasi ya tisa), Mwanza (nafasi ya tano kutoka nafasi ya
sita).
Mkoa wa Njombe uliokuwa kwa kwanza mwaka 2016, mwaka jana umeporomoka hadi nafasi ya 15.
Mkoa wa Iringa ulishika nafasi ya pili mwaka 2016, lakini mwaka jana
umeporomoka hadi nafasi ya 17 huku Kagera ulioshika nafasi ya tatu,
ukishuka hadi nafasi ya tisa.
Mkoa ulioshika mkia katika mpangilio huo ni Kaskazini Unguja uliotoka
nafasi ya 29 mwaka juzi hadi nafasi ya 31 mwaka jana, ukifuatiwa na
Kusini Unguja ulioshika nafasi ya 30 ambayo pia uliishika mwaka juzi.
Mikoa mitano iliyoshika mkia ni Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba, Kusini Pemba na Lindi.