Jumatano, 31 Januari 2018

MAGAZETI YA LEO 31/1/2018























Hii ndio gharama ya passport za kielektroniki



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt.  Mwigulu Nchemba amesema kuwa gharama mpya ya hati ya kusafiria ya kielektroniki itakuwa Sh. 150,000.

Dk Nchemba amesema hayo leo  wakati wa uzinduzi wa Hati ya kusafiria ya kielektroniki jijini Dar es Salaam ambapo imezinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Aidha Dkt. Miwgulu Nchemba amesema kuwa Pasipoti hizo zitakuwa na ukurasa zaidi ya mmoja  na mwonekano mpya.

“kiasi cha gharama hiyo  ni sawa na Sh15,000 kwa mwaka kwa sababu itatumika kwa miaka 10. Gharama za kupata pasipoti sasa ni TSh.50,000 na hutumika kwa miaka 10 tangu zilipotolewa,“ amesema Dkt. Mwigulu.

Hata hivyo Rais Magufuli amesema kuwa gharama ya laki moja na nusu bei hiyo ni ya juu kidogo kuliko bei ya sasa . huku kieleza kuwa bei hiyo imezingatia ubora wa utenngenezaji wa Pasipoti hiyo.

Rais Magufuli amwaga Bilioni 10 idara ya Uhamiaji



 John Magufuli leo January 31, 2018 ametangaza kutoa Tsh Bilioni 10 kwa Idara ya Uhamiaji ambayo iko chini ya Wizara ya Mambo ya ndani ili ijenge Makao Makuu yake Mjini Dodoma.
Rais Magufuli ametangaza kutoa pesa hiyo katika tukio la uzinduzi wa hati ya kusafiria ya kielektroniki Dar es Salaam na kueleza kuwa amefanya hivyo kama shukrani yake kwa Idara hiyo kwa jinsi ya utendaji wake siku za hivi karibuni.
“Dr. Makakala katafute eneo, nitawapa Tshs Bilioni 10, wakati wowote mtakapozihitaji muanze kujenga Makao Makuu ya Uhamiaji, na ninatoa hizi kama shukrani kwa kazi kubwa unayofanya wewe na watendaji wako.” – Rais John Magufuli.

Jumapili, 28 Januari 2018

#VPL Msimamo wa VPL baada ya mechi za leo: Simba 4 Majimaji 0 Singida United 1 Tanzania Prisons 0

No automatic alt text available.

#VPL Simba wanapata bao la 3 kupitia kwa kinara wao wa mabao, Emmanuel Okwi.

No automatic alt text available.

chadema wapata pigo tena jimbo la siha



Viongozi wote wa CHADEMA Kata ya Ormelili Wilaya ya Siha, Mkoa wa Kilimanjaro wanadaiwa kujiuzulu nafasi zao kwenye chama hicho nakuomba kujiunga na CCM.
Viongozi hao wamepokelewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Polepole wakati wa Kampeni za kumnadi mgombea Ubunge kwa tiketi ya CCM , Jimbo la Siha Dk. Godwin Mollel.
Miongoni mwa viongozi hao ni pamoja na aliyekuwa amejitolea nyumba yake kutumika kama Ofisi ya CHADEMA, Kata ya Ormelili, Janneth Mamboleo Mushi ambao kwa pamoja wameomba kujiunga na CCM na kuchukua nyumba yake.



#VPL Nahodha John Bocco anaiandikia Simba bao la pili kwa kuunganisha kwa kichwa krosi ya Said Ndemla ikiwa ni dakika 10 tu baada ya kufunga bao la kwanza.

No automatic alt text available.

#VPL Simba wanapata bao la kuongoza kupitia kwa nahodha wao, John Bocco anayetumbukiza mpira wavuni kwa kichwa.

No automatic alt text available.

SASA NI MAUAJI YA KIMBARI DHIDI YA JAMII YA WATUTSI:



Umoja wa Mataifa (UN) umepitisha kwa kauli moja uamuzi wa kubadili jina la mauaji ya Rwanda kwa kupewa jina la 'mauaji ya kimbari dhidi ya jamii ya watutsi'.
Awali mauaji hayo yalikuwa yakiitwa mauaji ya kimbari ya Rwanda kama ambavyo imekuwa ikifahamika.
Rwanda imepokea kauli hiyo kwa pongezi kutokana na mauaji hayo kuonekana mara nyingi yakipotoshwa kwa kuyataja kinyume na yalivyokuwa.
Katika mauaji hayo yaliyotokea mwaka 1994, UN inataja idadi ya watu laki nane ndiyo waliuawa huku serikali ya Rwanda ikishikilia watu waliouawa wakati huo walikuwa zaidi ya milioni moja.

Wimbi la wakimbizi wanaokimbia mapigano na ukatili nchini DRC


Wimbi la wakimbizi wanaokimbia mapigano na ukatili nchini DRC kuingia nchini Tanzania kupitia mkoani Kigoma limezidi kuongezeka na sasa inakadiriwa kufikia watu 1,200.

IBADA YA JUMAPILI:


 Rais John Magufuli aliyeambatana na mkewe Janeth Magufuli waliposhiriki ibada ya Jumapili katika Kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay,leo Jijini Dar es Salaam.

Baada ya Rais Magufuli, Rais Shein atoa msimamo wake kuhusu muda wa kukaa madarakani

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein amesema hayupo tayari kuongeza muda wa uongozi kutoka miaka mitano hadi saba kwani kufanya hivyo ni kukiuka katiba ya Zanzibar.

Dkt Shein amesisitiza kwamba, aliapa kuilinda katiba ya Zanzibar hivyo hawezi kubadilisha muda wa uongozi na hakuna mtu atakayemfanya abadilishe au amvutie yeye kuendelea kukaa madarakani.

Rais Dkt Shein ameyasema hayo jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume visiwani Zanzibar alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baaada ya kurejea kutoka kwenye ziara ya wiki moja katika nchi za Falme za Kiarabu (UAE) alipokua ameambatana na mke wake, Mama Mwanamwema Shein.

“Mimi naheshimu katiba ya Zanzibar, na nina heshimu sheria za Zanzibar. Muda wangu ukifika nitaondoka haraka sana. Hakuna atakayenilazimisha mimi nikae, au atakayenivutia mimi nikae” alisema Rais Dkt Shein.

Aidha, Dkt Shein amesema kuwa, alisikia wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi wakizungumza hilo, lakini hawazuiwi kujadili kwani wanafanya hivyo kwa mujibu wa sheria, lakini yeye hayuko tayari kuongeza muda.

“Hilo walizungumza wawakilishi barazani, wana haki ya kuzungumza, kwa mujibu wa taratibu zao na sheria zao na yeyote mwingine anaweza kuzungumza. Mimi nilisikia wakati wananzungumza, Mwakilishi mmoja akasema kwamba kuna baadhi ya nchi duniani zina miaka mitano nyingine saba, sasa kwanini na sisi tusiwe na miaka saba!”

Rais Dkt Shein amesema kuwa, suala la miaka saba labda linaweza kuwepo baada ya yeye kutoka lakini hadhani kama kuna jambo kama hilo.

“Mie sijalisema, sitolisema, na hakuna atayanilazimisha niliseme” alihitimisha Rais Dkt Shein, huku akitilia mkazo kwamba, muda wake ukiisha atamchukua mkewe na kumwambia waondoke.

wanafunzi watakiwa kuongeza juhudi ya masomo nchini




wanafunzi kote nchini wametakiwa kufanya biii katika masomo yao ili  kutimiza malengo yao katika maisha  ,rai hiyo imetolewa na  mkurugenzi  wa tasisi binafsi ya wezesha trust fund , lusako mwakiluma  mjini morogoro  , alipotembelea na kufundisha mbinu za kufanikiwa kwa wanafunzi  na stadi za maisha katika sekondari uluguru iliyopo kihonda mjini morogoro .

mkurugenzi huyo amesema kuwa ni vyema wanafunzi wakajitambua nini wanatakiwa kufanya wakiwa katika masomo shuleni badala ya kuingia katika makundi  mabaya , na badaye kujutia makosa.kwa kutotimiza malengo na ndoto zao.
 
''vijana maisha ni nyinyi wenyewe na kama wenyewe amtajikubali na kupambana na hali zenu mkasubiri kusukumwa hakuna litakalotokea''alisema, Madam Lusako nakuongeza kuwa ''kuzaliwa na famiia masikini au kupitia changamoto ni moja katika hali ya maisha ya binadamu yoyote, kijana amua kubadilisha maisha ya familia yako leo kwa kujitambua na kujihakikishia utakuwa wa kwanza katika familia kuondoa umaskini na kufanikiwa sana. Hakuna lisilowezekana kauli mbiu ni (Work Hard, Work Smart then Trust God). alisema lusako mwakiluma.
pia wanafunzi hao wa kidato cha nne katika sekondari ya uluguruWalifundishwa mbinu kumi zenye tija kwa weledi wa hali ya juu. katika kufikia malengo ya kufaulu mitihani yao.

kwa upande wake mwalimu wa shule hiyo bi bukuku amewashukuru wezesha trust fund kwakufika katika shule hiyo na kuweza  kutoa   darasa la stadi   za  maisha kwa wanafunzi hao wa kidato cha nne, nakuwataka  wanafunzi kuzingatia mafunzo hayo ,nakufuata ushauri waliopewa na na taasisi hiyo.

taasisi hiyo binafi ya wezesha trust imekuwa ikisaidia wanafunzi wenye mazingira magumu katika mkoa  wa morogoro  na mengine nchini tanzania .