Alhamisi, 30 Novemba 2017

Haji Manara kugombea Urais baada ya Rais Magufuli





Msemaji wa Klabu ya Soka ya Simba Haji Manara, amesema anampango wa kugombea urais na anaamini atafanikiwa.
Akiongea na Planet Bongo ya EA Radio, Haji Manara amesema kazi zake anazofanya sasa zimemfanya aache hesima kubwa, kitu ambacho kinampa ujasiri wa kufikia uamuzi huo.
“Unajua mi nakwenda kuwa rais wa nchi siku moja, mimi nakwambia Mungu akinipa uhai na majaliwa, nakwenda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”, amesema Haji Manara.
Msikilize hapa chini na akitaja watu gani hatawaweka kwenye baraza lake la mawa




Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Novemba 30

Jumatano, 29 Novemba 2017

Eto’o afafanua kuhusishwa kutoa fedha kwa waliyokwama Libya



Nahodha wazamani wa timu ya taifa ya Cameroon na mshambuliaji wa FC Barceloma, Samuel Eto’o amekanusha tuhuma za kuwapatia fedha raia wa nchi hiyo ambao walikuwa wamekwama Libya na kuelezwa kuwa wamekuwa wakiuzwa kama watumwa.

 Kupitia mitandao yake ya kijamii ya Instagram na Facebook Eto’o amekanusha vikali juu ya tuhuma hizo na kuwasihi watu kuonyesha upendo zaidi kwakuwa ndiyo kitu pekee kinachoweza kupambana na maovu na wala sio fedha.



Mshambuliaji huyo amehusishwa kuwaokoa Wacameroon waliyokuwa wamekwama Libya na kuwalipia usafiri wa ndege huku ikielezwa kuwa atatoa fedha kwa kila raia wa nchi yake aliyeokolowa.
“Several sites have circulated a rumor that I would have given money to every migrant returnee, in relation to a topical issue. This rumor is absolutely unfounded!”
“I would therefore take advantage of this opportunity, dear brothers and sisters, to emphasize that love prevents more evils than money can solve.”
“So let’s not waste our precious time looking for thrills at the expense of grieving people, but let us use this time to prevent other brothers from being deprived of their dignity.”
“Let us not just react when we can prevent, because among these victims are certainly people who have been our neighbours at some point, but to whom we have not daigné to look kindly. Let us build our Africa by having a positive impact on each other!.”

Rais wa Nigeria atoa neno kuhusu soko la watumwa Libya ‘Watu wangu wanauzwa kama mbuzi”

Tokeo la picha la buhari

 Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari amesema raia wote wa Nigeria ambao wamekwama Libya watarejeshwa nyumbani na kusaidiwa kurejelea maisha ya kawaida kwani nchini humo wamekuwa wakiuzwa kama Mbuzi.


Akizungumzia video za karibuni ambazo zimekuwa zikiwaonesha Waafrika wakiuzwa kwenye mnada wa watumwa nchini Libya, Rais Buhari amesema inasikitisha sana kuona “baadhi ya raia wangu wa Nigeria wanauzwa kama mbuzi kwa kiasi cha dola kadhaa nchini Libya”.
Ameonekana pia kushangaa iwapo raia wa Libya walijifunza lolote la maana tangu kuondolewa madarakani kwa Kanali Muammar Gaddafi mwaka 2011.
Walichojifunza pekee ni kuwapiga watu risasi na kuua. Hawakujifunza kuwa mafundi wa umeme, mafundi wa mabomba au ufundi wowote ule,” amesema Buhari.
Kwenye video iliyotolewa na CNN mapema mwezi huu, vijana kutoka mataifa ya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara walionekana wakiuzwa kama wafanyakazi wa mashambani kwa wanunuzi.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Buhari ameapa kupunguza idadi ya raia wa Nigeria wanaolazimika kufunga safari ndefu na hatari kupitia jangwa la Sahara na bahari ya Mediterranean kufika Ulaya.

Ndoa ya Dogo Janja na Irene Uwoya yaanza kuyumba





Kwa habari za kunyapia nyapia ni kwamba Irene Pancras Uwoya (Sheila Abdul) aanza kumchukia dogo janja kiasi cha kuyumbisha penzi lao na mbaya zaidi amekuwa akimnyima penzi dogo janja na mara nyingi hupenda kumkwepa kwepa janjaro na kiasi fulani anahisi kama janjaro ndo chanzo cha mumewe kipenzi Hamadi Kataut.

Dogo janja mara kwa mara akitafutwa kujibu suala hili la kunyimwa penzi na uwoya amekuwa akibabaika sana na muda mwengine hupenda kujibu nje ya mada ili asiendelee kuulizwa.

Katibu wa Chadema Simanjiro ajiunga Ccm



 Simanjiro. Katibu wa Chadema Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, Meshack Tureto amejiengua ndani ya chama hicho na kujiunga na CCM.

Tureto aliyekuwa pia katibu wa mbunge wa Simanjiro, James ole Millya ametangaza uamuzi huo akidai Chadema imepoteza dira na mwelekeo wa uongozi.

Anakuwa kiongozi wa pili wa Chadema wilayani Simanjiro kujiuzulu baada ya Jumamosi Novemba 25,2017 katibu wa uenezi, Ambrose Ndege kujiuzulu wadhifa huo na kujiunga na CCM.

Ndege alikabidhi kadi ya Chadema kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Akizungumza na MCL Digital leo Jumatano Novemba 29, Tureto amesema amefikia uamuzi baada ya kuona viongozi wenzake hawana mikakati wala mipango ya maendeleo.

Tureto amesema awali, alikuwa mtendaji wa Kijiji cha Narakauwo kilichopo Kata ya Loiborsiret kwa tiketi ya CCM lakini aliacha na kufuata mabadiliko Chadema.

Amesema chini ya uongozi wa Rais John Magufuli, mambo yanakwenda kama alivyotarajia hivyo hana sababu ya kuendelea kuwa Chadema.

"Chadema imepoteza mwelekeo sasa, nimeona nirudi CCM ambako hakuna kujilimbikizia vyeo na kila mwanachama ana haki kwa kuwa hii ni CCM mpya," amesema Tureto.

Amesema hakuingia Chadema kwa lengo la kupata masilahi bali alijiunga kwa utashi wake kama ambavyo sasa ameondoka na kurudi CCM.

Mbunge wa Simanjiro, James ole Millya amemtakia Tureto heri anakokwenda. Amesema sababu alizotaja za kuondoka Chadema hazina mashiko.

Ole Millya amesema Tureto aliingia Chadema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 baada ya kuona yeye ana nafasi kubwa ya kuwa mbunge wa Simanjiro.

Amesema Tureto alikuwa mtendaji wa Kijiji cha Narakauwo na alifukuzwa hivyo aliomba apatiwe nafasi naye akamjibu hana sifa.

Ole Millya amesema Tureto hakuwa katibu wa Chadema aliposhinda ubunge mwaka 2015 bali Frank Oleleshwa ambaye miezi sita iliyopita alipojiuzulu ndipo naye akashika nafasi hiyo.

"Wengi wanatafuta mafanikio binafsi na utajiri, lakini ukweli utabaki palepale CCM haitatawala milele Tanzania," amesema Ole Millya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Jackson Sipitieck amempongeza Tureto kwa kujiunga na chama hicho na amemhakikishia ushirikiano wa kutosha.

“Ipo siku nitakufa, hakuna anayeishi milele” – WEMA SEPETU



2017 muigizaji kutokea Bongomovie Wema Sepetu ameamua kuandika dukuduku lake kuhusiana na matusi ambayo amekuwa akitukwana kwenye mitandao ya kijamii jambo ambalo limemfanya aseme anatamani kutokuendelea kuwepo kwenye mitandao hiyo.
Wema ametumia ukurasa wake wa Instagram kuandika ujumbe huo na kuonesha jinsi gani amechoshwa na hali hiyo. Kwenye akaunti yake hiyo Wema ameandika….>>>”Ipo siku nitakufa, hakuna anaeishi milele… Sijui mtaendelea kunisema kwa kejeli na kunitukana matusi ya nguoni au ndo itakuwa, “Maskini ya Mungu, Dada wa watu alikuwa hivi na vile, Mungu ailaze Roho yake mahali pema…” Kuna muda mwingine huwa natamani Allah Subhannah wata’allah anichukue tu…
“Ya Duniya ni mengi sana…. Kuna muda mwingine nakufuru mwenyezi Mungu na kutamani labda hata nisinge exist… Ila acha niendelee kumtegemea yeye… Kila jambo hutokea kwa sababu…. Hili nalo litapita… I think I need a Time Off Social Media… Kwa mara nyingine Tena…. Siwezi jamani…” – Wema Sepetu

 

Akata nyeti za Mwanae kwa madai yakufukuza Mapepo mabaya



 MTU mmoja huko mwenye umri wa miaka 39 huko Chhattisgarh, India, amemtoa kafara mwanaye mdogo katika kitendo cha ushirikiana kwa kumkata uume na sehemu za kichwa kwa shoka hadi kusababisha kifo chake, kwa madai ya kufukuza mapepo mabaya ‘mashetani’.




 Kitendo hicho kilifanyika huko Balodabazar wilayani Chhattisgarh, polisi walisema jana. Ramgopal Patel, na mganga wa kienyeji, Rajesh Yadav (19) walikamatwa leo, ikiwa ni siku mbili baada ya kufanya kitendo hicho kijijini Amera.

Polisi walisema mwili wa mtoto huyo mwenye umri wa miaka 13 ulikutwa ukiwa katika dimbwi la damu ambapo baada ya polisi kufanya uchunguzi, Patel alikiri kumwua mwanaye huyo ili kuondoa mapepo mabaya na hivyo wamemfungulia mashitaka.

Rasmi: Kesho Alikiba katika ngoma Mpya



Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Alikiba siku ya kesho anatarijiwa kusikika katika ngoma mpya ambayo ameshirikishwa na Abdu Kiba.

 Pengine Alikiba kusikika katika ngoma hiyo inaweza isiwe stori, ila stori ni kwamba ngoma hiyo ni kwanza kutoka katika label ya Alikiba ‘King’s Music’ ambayo hapo awali alitangaza ujio wake.
Ngoma hii inakuja miezi mitatu tangu tangu Alikiba alipotoa ngoma yake ya kwanza kwa mwaka huu ‘Seduce Me’ ambayo mikono ya producer Man Water ilihusika, hata hivyo ngoma hii mpya ambayo video yake imeongozwa na Hanscana producer Man water kahusika tena.

Hii siyo ngoma ya kwanza kwa Alikiba kufanya na Abdu Kiba, utakumbuka walishafanya ngoma kama Kidela, Kajiinamia na nyinginezo.

Kenya, Tanzania katika mzozo mpya wa maji



Dar/ Nairobi. Ukanda wa hifadhi za Taifa za Serengeti na Maasai Mara nchini Kenya ambao una mojawapo kati ya maajabu manane ya dunia yanayovutia watalii, unakumbwa na tishio la kimazingira kutokana na nchi hizo mbili kuingia katika mgogoro wa kugombania maji.

Ajabu lililopo baina ya hifadhi hizo ni lile la kuhama kwa wanyama waitwao nyumbu.

Mvutano huo mpya unaibua mgogoro kati ya nchi hizo jirani ambazo ni vigogo ndani ya Jumuiya Afrika Mashariki (EAC).

Mgogoro huo unatokana na uamuzi wa Serikali ya Kenya kujenga mabwawa mawili katika Mto Mara ambayo wataalamu wanaonya kuwa yatakausha ukanda huo na kuathiri uzao wa ndege katika Ziwa Natron, huku Tanzania ikipanga kuvuna maji katika mto huo na kuufanya usitiririshe ipasavyo maji yake katika Ziwa Victoria.

Kenya inatarajia mradi huo utasaidia kumwagilia mashamba karibu na chanzo cha mto huo katika Msitu wa Mau na kumaliza tatizo la maji kwa wakazi wa maeneo hayo. Hata hivyo, wataalamu wa mazingira wanaeleza kuwa hatua hiyo itaathiri zaidi upatikanaji wa maji ukanda mzima hasa mwisho wa mto huo na madhara hayo kuathiri hadi Tanzania.

Mto Mara ni maarufu duniani kutokana na wanyama hao kuuvuka hususan uhamaji wao wa kila mwaka kutoka upande mmoja wa nchi kwenda mwingine.

Kati ya Julai na Septemba kila mwaka, idadi kubwa ya nyumbu huwasili katika kingo za mto huo na hujikusanya kwa muda katika eneo hilo na baadaye huanza safari ya kuhamia upande wa pili kwa kuchagua sehemu moja ya kuvukia katika mto huo.

Kitendo cha wanyama hao kuhama kila mwaka kwa kujikusanya kwa pamoja na kujitupa kwenye mto wenye mamba lukuki ili kuvuka upande wa pili, kimelifanya tukio hilo kuwa ni moja ya maajabu manane yaliyopo duniani.

Inakadiriwa kuwa nyumbu takriban milioni 1.5 wakisindikizwa na kundi kubwa la pundamilia, pofu, swala na digidigi huhama kila mwaka kutoka Serengeti Tanzania na kwenda Hifadhi ya Maasai Mara nchini Kenya katika jitihada za kutafuta chakula.

Asili ya mvutano huo wa maji upo katika mpango kazi wa mwaka 2002 wa Kenya unaopanga kuhamisha kiwango kikubwa cha maji kutoka Mto Emala kwenda Ewaso Ngiro katika eneo la chanzo cha maji cha Bonde la Ufa.

Ripoti ya Mamlaka ya Usimamizi wa Maji ya Mpango wa Uhamishaji wa Maji, Bonde la Mto Mara ya Kenya (2017-2022) inaeleza kuwa umwagiliaji utakunywa kiasi kikubwa cha maji kutokana na kutumia kati ya asilimia 70 hadi 80 ya maji yote. Jambo hilo limewavuta wanamazingira wa Tanzania walioeleza ujenzi huo wa mabwawa Kenya utasababisha madhara makubwa katika mazingira ya Serengeti, huku wakitanabaisha kwamba asilimia 75 ya ndege aina ya flamingo wadogo huzaliwa maeneo ya Ziwa Natron.

Hata hivyo, kaimu mkurugenzi anayeshughulikia masuala ya maji yanayohusu nchi mbili wa Kenya, Gladys Wekesa anasema hadi sasa ujenzi wa mabwawa hayo haujaanza na hawana mpango wa kuhamisha maji yote kutoka Mto Mara na kwamba, mradi huo unafanywa kwa kuzingatia masilahi ya pande zote mbili.

Wekesa alisema Bwawa la Amala ni sehemu ya mpango wa uendelezaji rasilimali maji wakati lile la Norera linalotarajiwa kuendesha mradi mdogo wa umeme wa kilowati 90 litakuwa na ukubwa wa mita za ujazo 450,000.

Alisema mradi huo ulipangwa na kukubaliwa na pande zote mbili lakini anashangaa kuona maofisa wa Tanzania wanageuka.

Hata hivyo, Bakari Mnaya na Mtango Mtahiko wa Mamlaka za Hifadhi za Taifa (Tanapa) pamoja na Profesa Eric Wolanski wa Chuo Kikuu cha James Cook cha Australia wanasema katika ripoti yao kuwa, kutokana na kiwango cha maji kilichopo mahitaji ya sasa yanaweza kutimizwa bila kuharibu hifadhi ya maji.

Katika ripoti hiyo wanaeleza kuwa hakuna uhakika kuwa maji yaliyopo yatatimiza mahitaji ya baadaye hususan kipindi cha kiangazi kikali iwapo nchi zitaendelea kuendeleza miradi mikubwa inayotumia maji mengi.
 

IGP Sirro awataka watoto wa Kibiti



 Mkuu wa jeshi la polisi nchini (IGP) Simon Sirro amewataka wazazi na walimu wilayani Kibiti na Rufiji, kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola juu ya kutoweka kwa wanafunzi zaidi ya 1,300 wakati wa matukio ya kiuhalifu yaliyotokea katika wilaya hizo.

Katika ziara yake ya kikazi wilayani Kibaha, mkoani Pwani IGP amezungumza na wazazi, walimu pamoja na viongozi wa mashirika ya umma,wazee maarufu, wastaafu mbalimbali na kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo.

IGP Sirro amewataka wazazi husika na walimu wa shule za msingi na sekondari ambazo wanafunzi walikuwa ni watoro ama hawajaripoti shule kwa miezi kadhaa kutoa taarifa kwani wapo baadhi ya watoto wanaotumika kufundishwa uhalifu hata wakutumia silaha na watu wasiowema.

Kamanda Sirro ameeleza kuwa taarifa ya wanafunzi zaidi ya 1,300 mkoani hapo kuwa ni watoro na hawajulikani walipo hivyo wazazi washirikiane kusaidia jeshi la polisi kujua walipo.

“Kuna baadhi misikiti,makanisa yanadaiwa yanayotumia watoto hawa katika masuala ya kiuhalifu hivyo kuna kila sababu ya kuingia ndani kutafuta suluhu”, amesema Sirro.

Mkuu huyo wa jeshi la polisi amewahakikishia wananchi mkoani Pwani kuwa silaha zote zilizochukuliwa na wahalifu wa ovyo ovyo huko Kibiti na Mkuranga zimerudi zote mkononi mwa dola na kusambaratisha mtandao wa kiuhalifu na wanaendelea kushirikiana na Msumbiji kutokomeza uhalifu.

Waziri Mkuu aagiza kukamatwa kwa waliotaka kutoa bandarini Semi tela 44


 Waziri Mkuu. Kassim Majaliwa (mwenye Tai nyekundu) amefanya ziara ya kushitukiza katika Bandari ya Dar es salaam leo November 29, 2017 na kubaini Kampuni ya NAS ikitaka kutoa Semi Trela 44 bila ya kufuata utaratibu.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro kuwakamata, Bw. Bahman wa kampuni ya NAS na Wakala wa Kampuni ya Wallmark Bw. Samwel kwa kutaka kutoa bandarini magari makubwa aina ya semi tela 44 bila ya kulipa kodi kwa kutumia jina la Waziri Mkuu.

Pia Waziri Mkuu ameitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kutowasikiliza wafanyabiashara wanaotaka kukwepa kodi kwa madai ya kupewa vibali vya msamaha wa kodi kutoka kwa viongozi wa juu Serikalini.

“Mtu asije hapa aseme amepewa kibali na Rais Dkt. John Magufuli, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan au Waziri Mkuu cha kutaka kutoa mzigo wake bila ya kufuata taratibu. Akija mtu na taarifa hizo akamatwe mara moja na achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.”

Ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Novemba 29, 2017) alipofanya ziara ya ghafla bandarini baada ya kupata taarifa za mfanyabiashara huyo aliyetaka kuutapeli uongozi wa TPA kutaka kutoa magari hayo yaliyoingizwa nchini mwaka 2015 kutoka nchini Uturuki.


Hatua hiyo imekuja baada ya Bw. Bahman wa kampuni ya NAS kutaka kupata msamaha wa kodi kwa kuidanganya TPA kwa madai kwamba wamewasiliana na Waziri Mkuu na wasipotekeleza jambo hilo watapata matatizo.

Amesema Serikali inasisitiza watu kufuata sheria na taratibu za nchi ikiwa ni pamoja na kulipakodi ipasavyo na inataka watendaji wake wafanye kazi bila ya kubugudhiwa, hivyo amewataka wafanyabiashara kufuata sharia za nchi na kwamba Serikali haina ugomvi nao. Waziri Mkuu amefafanua kuwa mfanyabiashara huyo alitaka kuyatoa magari hayo bila ya kukamilisha malipo ya ununuzi kutoka kwenye kampuni Serin ya nchini Uturuki.

“Magari haya aliyalipia asilimia 30 tu kwa makubaliano ya kumaliza asilimia 70 iliyobaki baada ya kufika Tanzania na atakapokamilisha ndipo angepewa nyaraka ambayo inaonyesha jina la mwenye mzigo, aina ya mzigo na thamani (bill of lading) inasaidia mteja kufanyiwa tathmini ya gharama za kulipia ushuru, lakin huyu bwana hajafanya hivyo”

Waziri Mkuu amesema kitendo cha kuyasajili magari hayo bila ya kuwa na nyaraka hizo ni kinyume cha sheria na pia kinaweza kusababisha kampuni iliyouza magari hayo ya Serin kutolipwa malipo yaliyobaki.

Amesema jambo hilo halikubaliki kwa sababu linaweza kudhohofisha mahusiano mazuri iliyopo kati ya Tanzania na Uturuki kwani tayari kampuni hiyo imeshawasilisha malalamiko hayo katika ofisi za Ubalozi wa Uturuki nchini Tanzania.

“Uturuki wanawaamini sana wafanyabiashara wa Tanzania sasa huu ujanjaunja uliotumika katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kuyasajili magari haya bila ya kuwa na bill of lading halisi unajenga sura mbaya kwa wafanyabiashara wengine waaminifu na watiifu wa sheria nawaagiza TRA kuchukua hatua kwa wahusika, hatuwezi kupoteza mahusiano na nchi kwa sababu ya utapeli wa mfanyabiashara mmoja.”

Pia Waziri Mkuu ametoa wito kwa Mawakala wa Forodha kuhakikisha wanakuwa makini katika kazi zao na Serikali haitawavumilia wababaishaji kwani inasisitiza wafanyabiashara kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo.

Awali, Mkurugenzi wa Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko alimueleza Waziri Mkuu kuwa pamoja na vitisho vya mfanyabiashara huyo kuwa wasipotekeleza matakwa yake watapata matatizo, lakini waliendelea kusimamia sheria na taratibu.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU JUMATANO, NOVEMBA 29, 2017.​

Malaria yaleta hofu- Ripoti



Idadi ya wagonjwa wa Malaria kwa mwaka 2016 iliongezeka kwa zaidi ya visa milioni 5 ikilinganishwa na mwaka 2015 na hivyo kutiwa hofu juu ya mafanikio yaliyopatikana katika kutokomeza ugonjwa huo.
Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya shirika la afya ulimwenguni, WHO iliyotolewa Jumanne ikiongeza kuwa hata idadi ya vifo vitokanavyo na Malaria vimesalia 445,000 ikiwa ni sawa na mwaka 2015.
WHO inasema kwa hali ilivyo sasa, dunia iko njiapanda na ni lazima hatua ichukuliwe ili kuepusha kurejea katika hali ya zamani na hivyo kushindwa kufikia lengo la kutokomeza Malaria ifikapo mwaka 2030.





Moja ya sababu iliyotajwa katika mkwamo wa kudhibiti Malaria ni upungufu wa ufadhili ambapo tatizo kubwa ni kupata fedha kutoka vyanzo vya ndani ya nchi na hata kimataifa ili kununua vyandarua vyenye viuatilifu, dawa na vifaa vingine vya kukabiliana na Malaria.
Akizungumzia kutokupungua kwa visa vya Malaria, Dkt. Winnie Mpanju Shumbusho, ambaye ni mwenyekiti wa ubia wa kutokomeza Malaria duniani, RBM ameieleza idhaa hii kuwa.