Mwili wa marehemu ukielea mtoni huku ukiwa kwenye viroba.
MWILI wa mmiliki wa mabasi ya Super Sami, Samson Josiah, unadaiwa
umekutwa na wavuvi mto Ndabaka eneo la Bunda – Lamadi akiwa amefariki
dunia jana Jumatano, Machi 14,2018 jioni huku watu wa karibu na marehemu
wakithibitisha kuwa mwili huo ni wake.
Machi 9, 2018 taarifa za kupotea kwa Josiah kwa zaidi ya wiki mbili
zilianza kusambaa baada ya gari lake alilokuwa akitumia aina ya Toyota
Land Cruiser kukutwa limechomwa moto katika Hifadhi ya Taifa ya
Serengeti iliyoko mkoani Mara huku akiwa hajulikani alipo.
Global Publishers imemtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Jafary Mohammed, ambaye amethibitisha kupokea taarifa hizo.
“Hata mimi nimesikia tu taarifa za kuokotwa kwa mwili wa Samson Josiah,
sasa hivi ndiyo ninaelekea eneo la tukio ili kufahamu kilichojiri, kama
ni yeye aliyeokotwa au ni mwingine. Lakini taarifa za kupotea kwake
zilitufikia na tulizitoa kwa umma siku chache zilizopita, hivyo tuwe na
subira, tutawaeleza baada ya kupata taarifa kamili,” alisema RPC.
Gari lake likiwa limeteketea kwa moto.
Kwa mujibu wa familia ya Josiah, ambayo inaishi mkoani Mwanza, ilidai
kuwa siku ya kupotea kwa kwake ambayo ni Februari 27, majira ya usiku,
alimpigia simu mkewe na kumwambia kuwa atarudi nyumbani na mgeni, na
hayo yakawa mawasiliano yao ya mwisho.
Mabasi ya Super Sami yanafanya safari zake kuanzia mkoa wa Mwanza, kwenda mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa na Kagera.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni