Wananchi hao wamesema tangu mwaka 1974 walipotumia maji kwa mara ya mwisho kwa sasa wanatumia maji ya visima na mtoni ambapo kipindi cha kiangazi maji hukauka kwenye visima huku wakati wa masika maji ya visima huchafuka kwa maji machafu kuingia ndani ya visima hivyo.
Hata hivyo wakati wananchi hao wakitoa vilio vyao hivyo, Naibu waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso amewasili wilayani Malinyi kushuhudia maendeleo ya mradi mkubwa wa maji unaotarajiwa kumaliza tatizo hilo la muda mrefu kwa wakazi hao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni