KOCHA Mkuu wa Al Masry, Hossam Hassan akiri kuifahamu Simba vizuri kwa kuwa ametumia muda mwingi kuangalia video za mechi zao lakini hofu yake imekuwa kwa Emmanuel Okwi.
Hossam ambaye ni mchezaji wa zamani wa Misri na Zamalek alikutana Simba mwaka 2003, katika Ligi ya Mabingwa Afrika akiwa mchezaji na timu yake kuondoshwa kwa penalti na Simba kutinga makundi ya michuano hiyo mikubwa Afrika.
Hossam alisema; “Wapinzani wetu tunawaelewa vizuri kwa sababu tumetumia muda mwingi kuangalia video za mechi zao lakini wametutisha kidogo kwenye ushambuliaji kwa kuwa wanaonekana wao ni bora sana.”
“Pale wana wachezaji wazuri sana, lakini tutajitahidi kukabiliana nao wasituletee madhara,” alisema Hossam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni