
Rais mpya wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amefanya mabadiliko
"muhimu" kwenye baraza la mawaziri ikiwa ni uamuzi wa kwanza mkubwa
kuufanya tangu kutwaa madaraka hayo.
Ramaphosa amemrudisha kwenye
uwaziri wa fedha, Nhlanhla Nene (aliyeondolewa kwenye nafasi hiyo na
aliyekuwa rais wa nchi hiyo Jacob Zuma), pia amemteua David Mabuza kuwa
makamu wa rais (Mabuza ni makamu mwenyekiti wa ANC) na amemteua
aliyekuwa mpinzani wake kwenye kuwania uenyekiti wa ANC, Nkosazana
Dlamini-Zuma kuwa waziri kwenye ofisi ya rais.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni