Timu hizi mbili mwaka 2014 zilikutana katika fainali ya Ngao ya Hisani ambapo Arsenal waliichapa Man City bao 3-0 lakini pia wakakutana katika mchezo wa nusu fainali ya FA ambapo Gunners waliichapa tena City bao 2-1.
Mara nyingi timu hizi mbili zimekutana katika mechi za EPL na rekodi zinaonesha katika mechi 5 zilizopita kati ya Arsenal na City katika EPL, City wamepoteza mara moja tu lakini wakashinda mara 2 na pia wakapata suluhu mara 2.
Katika kikombe hiki cha ligi ukiacha mara mbili ambazo City wameifunga Arsenal (2009/2010 na 2011/2012) ,lakini kabla ya hapo Manchester City hawajawahi kuwafunga Arsenal katika kikombe cha ligi kuanzia msimu wa 1977/1978 hadi msimu wa 2004/2005.
Kwa Arsenal hii ni fainali yao ya 8 na ndio klabu inaongoza kwa kupoteza fainali nyingi kwani katika fainali hizo wamepoteza fainali 5 za mshindano hayo na wakafanikiwa kushinda fainali mbili (1987 na 1993).
Hii leo itakuwa mara ya sita kwa Manchester City kucheza fainali ya kombe la ligi na itakuwa mara ya 3 katika misimu mitano iliyopita, katika fainali hizo Man City wameshinda fainali 5 na mara pekee waliyoshindwa ni msimu wa 1974.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni