Jumanne, 23 Januari 2018

NAFASI YA URAIS:



Chama cha ANC cha Afrika Kusini kimesema hakuna ratiba ya kumwondoa madarakani rais Jacob Zuma kwa sasa.
Chama hicho tawala nchini humo kimeongeza kuwa tayari kimeshajadili suala la kumwondoa madarakani rais Jacob Zuma wa nchi hiyo, lakini hakuna ratiba iliyopangwa kufanya hivyo hivi karibuni.
Katibu Mkuu wa ANC, Ace Magashule amesema kamati tendaji ya taifa ya chama hicho haijafanya uamuzi wa kumwita na kumhoji rais Zuma, ambaye anashinikizwa kujiuzulu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni