Alhamisi, 22 Juni 2017

Samaki Aina ya Electric eel Mwenye Uwezo wa Kuzalisha umeme.




Duniani yapo mengi ambayo yanavuta hisia ukiyasikia. Wengi wetu huamini kuwa umeme umekuwa ukizalishwa kutoka katika vyanzo mbalimbali kama mashine, betri, jua na maji.
 
Lakini amini au usiamini kuna viumbe ambao wanazalisha umeme mwingi wenye nguvu hata ya kuweza kumuua binadam mtu mzima ndani ya sekunde.
 
Moja ya viumbe wenye uwezo wa kuzalisha umeme ni samaki aina ya electric eel au electricus fish ambae ana umbo refu mfano wa bomba huwa akikuwa anaweza akafikia urefu wa mita 2 ( futi 6-7) na uzito wa kilo 20 kitu kinachomfanya kuwa samaki mkubwa katika kundi la Gymnotiformes
Samaki huyu ana rangi ya kahawia iliyokolea kwa upande wa nyuma(mgongoni) na rangi ya manjano au machungwa mbavuni na tumboni. Ana mdomo wenye pembe  ambapo pembe hiyo hujitokeza mwishoni mwa pua. 
 
Kama walivyo samaki wa kundi la ostariophysan, kibofu cha kuogelea kimegawanyika sehemu mbili, ndani ambapo kimeungana na sikio landani kwa kutumia mtililiko wa vifupa ambavyo vinatokea kwenye uti wa shingo ambao kitaalam unaitwa Weberian apparatus, ambao ndio unaomsaidia kupata uwezo wa kusikia.
 
Sehemu ya pili ni ile inayoanzia nyuma kuja mbele na inachukua karibu sehemu yote ya urefu wake na ndio inayomsaidia kuweza kuelea ndani ya maji. Samaki huyu ni lazima aje juu ya maji kila baada ya dakika kumi kupata hewa(kupumua) kabla ya kuludi chini ya maji. Karibia asimia 80 ya hewa ya oxygen anayoivuta anaipata kwa njia hii.
 
 
Electric eel ana viungo tofauti vinavyomsaidia kuzalisha umeme, cha kwanza kinazlisha umeme kwa ajili ya kuwindia na kingine kinazalisha kwa ajili kusikilizia. Viungo hivi vya kuzalishia umeme vinatengeneza 4/5 ya mwili wake wote, na vinmuwezesha kuzalisha umeme wa aina mbili ule wenye nguvu kubwa na ule wa nguvu ndogo. Viungo hivi ambavyo vimeundwa na elektroliti vimejipanga kwa pamoja ambapo ngunvu ya umeme inapita kama vile ufanyavyo kwenye waya.
 
Kipindi eel anapohisi windo ubongo wake hutuma taarifa kwenye elektroliti na hii hupelekea kufungua chaneli ya madini yachuma ambayo inaruhusu sodium kupita kwa kubadili mkondo kuludi nyuma ambapo mabadiliko ya haraka hutokea katika mkondo na kupelekea kuzalisha umeme kama vile betri ambapo seli hupangwa pamoja ili kupata umeme.
 
Ndani ya electric eel, baadhi ya  seli 5,000 mpaka 6,000 zilizojipannga kwa pamoja ambazo zina uwezo wa kuzalisha volt 860 na watt 860 ndani ya chini ya sekunde moja. Umeme huu una uwezo wa kumdhuru hata kumuua mtu mzima.
Pia ndani ya smaki huyu kuna ogani nyingine ijulikanyo kama Sach’s ambayo inaundwa na seli nyingi ambapo kila seli inazalisha umeme mdogo wa volti 0.5, organi hii inazalisha  umemewa 10V katika mawimbi ya 25hHz kwenda juu , ambapo huutumia umeme huu mdogo kwa ajili ya kufanya mawindo yake hasa ukizingatia kuwa hana macho.
Pindi  samaki huyu anapojihakikishia kuwa windo lake lipo ndani ya mzio wake basi huachia ule umeme mkubwa ambapo ukimpata windo basi hupoteza nguvu na hivyo kumezwa na samaki huyu.
 
Electric eels amekuwa akifanyiwa uchunguzi wa bioelectrogenesis. Na amekuwa ni kivutio kwa watafiti, ambapo watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Yale  nchini Marekani na wizara ya taifa ya teknolojia wanajalibu kuona kama wanaweza kutengeneza seli feki zinazofanana na za samaki huyu au kuboresha seli za samaki huyu. Uzalishaji ama uboreshaji wa seli hizo unaweza kuendelezwa kisayansi ili kuweza kuwa kama chanzo cha nguvu kwa viungo vya vya bandia na vifaa tiba.
 
Electric eels anaishi katika maji ya baridi(yasiokuwa na chumvi) katika msitu wa Amazon na  katika bonde la mto Orinoco  huko America kusini. Na maranyingi hupatikana katika kina cha mto katika maji yaliyotulia kiasi.
Chakula chake kikubwa ni wadudu, konokono, kaa, minyoo ingawa mala nyingine anaweza kula samaki na wanyama wadogo wadogo kama panya.
Uzalialianaji wake ni wa kutaga mayai kipindi cha kiangazi ambapo hutaga mayai karibia 3000. Samaki jike ndio mwenye umbo dogo kuliko dume.
 
 
chanzo vyote blog .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni