Jioni moja nikiwa nimeboreka nikaona itakuwa vema ikiwa nitafanya kutoka na kwenda kutembea tembea hapa na pale, kwakua makazi yangu yamejitenga na makazi mengine kwa kiasi kikubwa basi ni lazima ukatize kwenye vichaka vya hapa na pale, mbele yangu nikamuona mnyama mdogo mdogo akikatiza kama ananusanusa chini lakini kwa haraka…ikanibidi kusimama ili kuona kinachoendelea, kwanza niliona kama sungura au panya mkubwa na kwa jinsi nnavyoipenda nyama pori nikajisemea mboga ya jioni ya leo imejileta kirahisi namna hii hapa ni mwendo wa chui nakula mboga. Alivyojichomeka kichakani na kwa kuwa kicha kile nakifahamu vema sikupoteza muda nipo pale na gongo langu mkononi, la haula kwa karibu nikagundua nimekosea timing maana naweza kuwa windo la myama huyu…maana kumekuwepo na hadidhi kadhaa za kumhusu mnyama huyu maalufu kama nungunungu, asije nirushia mishale yake nikapoteza macho yangu huku bado nayapenda.
Lakini niashangaza na kuwa pamoja na kuniona hakuwa
na shida na mimi wala hakulusha miba yake na badala yake kwa mwendo uleule
akaingia shimoni na sikumuona tena,
nikabaki kuwaza kupo wapi kule kulusha miba mbona ni mpole hana madhara kwa
binadamu…kutokea hapo nikatamani kumjua huyu kiumbe ni wa namna gani?
Nungnungu au nungu ni ni
mnyama mgugunaji mwenye ngozi yenye miiba iliyochongoka wanayotumia kujilinda
na maadui,Ila sio kwa kuilusha miiba hiyo. Mnyama huyu mdogo
anayeishi milimani, mashambani, na msituni ni wa kipekee sana. Ana manyoya
magumu ya kahawia na meupe kichwani na shingoni, lakini miiba yake yenye ncha
za rangi ya manjano ndiyo humtambulisha zaidi. Miiba hiyo yenye urefu wa
sentimeta mbili hivi ni mikali na imepangwa katika makundi-makundi.
Miiba
ya kila kundi hukua kutoka mahali pamoja na kuufunika mwili wake. Kila mwiba
umezungukwa na mitaro-mitaro na umejipinda mahali ambapo umeshikamana na ngozi
na kufanyiza pembe-mraba. Mwiba huanza kuwa mwembamba na kujipinda unapokaribia
kushikana na ngozi. Ndiyo sababu nungunungu hawezi kuchomwa na miiba yake hata
akianguka kutoka mahali palipoinuka. Ama kweli, nungunungu ameumbwa kwa njia ya
ajabu!
Ni vigumu sana kuweza kumuona kwa vile anaishi
kwa mashaka sana,maana mara tu anapoonekana machoni pa watu hushambuliwa na
kuwaua kwa sababu mbalimbali.Wengine huwaua kwa sababu ya kuwatuhumu kuwa
wanakula mazao yao mashambani.Lakini wengine humuua kwa sababu wanadai kuwa
miiba yake ni dawa. Nungunungu hupenda kuishi na kufurahia mazingira yenye
mapori na misitu ili kujihadhali na ukatilii anaotendewa. Hupenda sehemu zenye nyasi ndefu ndefu ajili ya
usalama wake.
Anaposhtuliwa, nungunungu hujikinga kwa
kujikunja kama mpira. Misuli yake yenye nguvu hukaza ngozi yake yenye miiba na
kuufunika mwili wake mzima. Ngozi
hiyo yenye miiba hufunika kichwa, mkia, miguu, na sehemu zake za chini. Mnyama
huyo anaweza kujikunja hivyo kwa muda mrefu.
Nungunungu huona njaa wakati wa jioni. Chakula chake cha jioni huwa
wadudu na minyoo, lakini wakati mwingine anaweza kula panya, chura, mjusi, au
hata njugu na matunda ya beri. Nungunungu husikia vizuri sana. Pia ana uwezo wa
kunusa wenye nguvu, na unaweza kutambua jambo hilo ukiona pua lake refu lenye
umajimaji.
Mbali na mbweha na melesi, nungunungu hana
maadui wengi mwituni. Melesi aweza kubambua ngozi ya nungunungu kwa kucha zake
zenye nguvu bila kuumizwa na miiba. Nimewahi kuona ngozi ya nungunungu mara
kadhaa. Huenda ngozi hiyo ikawa imebaki baada ya melesi kumla nungunungu
mzima. Kwa upande mwingine, mbweha hawezi kustahimili miiba ya nungunungu,
lakini anaweza kujaribu kumviringisha hadi majini, ambapo nungunungu hulazimika
kujikunjua la sivyo atakufa maji. Kwa kuwa nungunungu ni mwogeleaji hodari,
huenda akafikia mawe au kuingia ndani ya mashimo yaliyo kando ya mto kabla
mbweha hajamnyakua na kumfanya kuwa kitoweo chake.
Nungunungu huanza
kujamiiana katikati ya miezi ya Mei na Julai, na wanarudia kufanya hivyo kwa
mara ya pili katika kipindi hichohicho. Baada ya majuma manne hadi sita, watoto
watatu au wanne huzaliwa wakiwa na uzito unaopungua gramu 30. Watoto hao huwa
hawaoni wala kusikia wanapozaliwa, hivyo wanaweza kushambuliwa kwa urahisi
katika majuma mawili ya kwanza. Kisha miiba humea mahali palipokuwa na manyoya
laini. Baadaye wanaweza kujikunja kabisa. Kabla ya kupata uwezo huo, wao huruka
juu mara moja na kutoa mlio mkali wa kuchatachata wanaposhtuliwa. Jambo hilo
huwashtua maadui zao wengi.
Wakati nungunungu amelala, yeye hutumia
mafuta aliyohifadhi mwilini katika miezi ya joto. Wakati huo joto la mwili wake
hupungua sana, naye hupumua kidogo sana hivi kwamba si rahisi kutambua kama
anapumua. Ana tezi maalumu anayotumia kudhibiti hali ya joto la mwili wake
anapolala. Kiasi cha joto kikipungua sana wakati huo, tezi hiyo hutokeza joto
zaidi linalomfanya ajue kwamba anapaswa kutafuta makao yenye joto zaidi,
yaliyozingirwa zaidi. Hii haimaanishi kwamba wakati wa baridi nungunungu hana
habari kuhusu kinachoendelea katika mazingira yake. Anaweza kusikia sauti
yoyote iliyo karibu naye, na kumfanya asonge kidogo.
Ukijaribu kumfuga nungunungu, yeye
hupanda ukutani, au kwenye bomba la maji na kuponyoka kwani anapenda kulisha
katika eneo kubwa. Ndiyo sababu, si rahisi kumfuga au kumfanya awe mnyama
kipenzi. Ni vizuri zaidi kwamba hafugwi kwa kuwa yeye hubeba viroboto wengi
sana
chanzo mtandao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni