Jumapili, 4 Februari 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya February 4

SeeBait

Mwanamke ajifanya muuguzi na kuiba mtoto wa siku moja Mbeya

Picha ya mtandao
Polisi mkoani hapa wanamsaka mwanamke ambaye aliyejifanya muuguzi na kuiba mtoto wa kike wa siku moja kwenye wodi ya wazazi katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.
Mtoto huyo alizaliwa kwa njia ya upasuaji na Sarah Mwasanga (40), mkazi wa Iganzo jijini hapa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohamed Mpinga alisema tukio hilo lilitokea juzi alfajiri kabla ya ndugu na jamaa kuingia kuona wagonjwa.
Mpinga alisema mwanamke huyo alifika hospitalini hapo kwa pikipiki huku akiwa amebeba kitu mithili ya mtoto na alipohijiwa na walinzi getini, alieleza ana mgonjwa ameandikiwa sindano za masaa hivyo akaruhusiwa kuingia.
“Alitumia mbinu ambayo kwa namna moja au nyingine ilifanikisha azma yake jambo ambalo hata wakati anatoka walinzi hawakumtilia shaka kwa kutambua tayari kapatiwa huduma,” alisema.
Mpinga alisema awali alipoingia kwenye wodi ya wazazi, aliwahoji kinamama waliojifungua kuwa anahitaji mtoto wa kike kwa ajili ya kumpatia chanjo, ndipo mzazi wa mtoto huyo alimkabidhi kwa kutambua ni muuguzi kutokana na mavazi aliyokuwa amevaa.
Alisema hilo ni tukio kubwa lililotokea mkoani hapa tangu aliporipoti na kwamba wanaendelea na uchunguzi.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Yahaya Msuya amekiri kutokea kwa tukio hilo, na kwamba kwa sasa lipo kwenye uchunguzi zaidi.
Mama wa mtoto huyo, Sarah Mwasanga aliomba msaada wa jeshi la polisi kufanya jitihada za haraka kuhakikisha mtoto wake anapatikana.

Jumamosi, 3 Februari 2018

Wasaka hifadhi 90 wafa maji pwani ya Libya



Watu wanaovuka bahari ya mediterranea kutoka Afrika kasakzini.(Picha:UNHCR)
Taarifa zilizotolewa leo na  Shirika la Umoja wa mataifa la uhamiaji IOM z inasema, wahamiaji 90 wameripotiwa kufa maji baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kupinduka na kuzama katika bahari mediteranea pwani ya Libya. Patrick Newman na maelezo kamili .
Shirika hilo linasema wahamiaji wanaendelea kupoteza Maisha kila uchao wajaribu kwenda kusaka mustakhbali bora. Kufuatia mkasa huo Bi Olivia Headon ambaye ni mwakilishi wa IOM Libya akizungumza  na wandishi wa habari kwa njia ya simu mjini Genevia  amesema..
(Sauti ya Olivia Headon)
Watu wapatao 90 wamekufa maji wakati boti waliokuwa wakisafiria kupinduka mapema hii leo ,miili ya wa watu 10 kati yao, wawili wakiwa  raia wa Libya na wanane  kutoka Pakistan imeokolea pwani ya Libya, wakati huohuo vikosi wa uokowaji vya Libya vimeripoti kuokoa watu wawili walioweza kuogelea hadi nchi kavu na mmoja kuokolewa na wavuvi bahari.
Kwa mujibu wa ripoti ya IOM ya mwaka jana zaidi ya wananchi 29 wa  Libya waliripotiwa kuokolewa wakijaribu kwenda kusaka hifadhi ughaibuni.
Halikadhalika wasaka hifadhi elfu tatu kutoka Pakistan wameripotiwa kuingia Italia kupitia Libya mwaka 2017, ikilinganishwa na 240 katika  mwezi wa januari 2018 .

Baba aiambia Mahakama “Naomba dakika 5 nifungiwe na shetani”



Baba wa mabinti watatu waliodhalilishwa kingono na Daktari wa Mazoezi wa Marekani, Larry Nassar amejaribu kumshambulia mbele ya mahakama ya Michigan, baada ya kumvaa mshtakiwa huyo anayetuhumiwa kudhalilisha wachezaji kadhaa waliopitia mikononi mwake.
Hata hivyo Randall Margraves hakufanikisha lengo lake hilo baada ya kudhibitiwa vyema na maofisa watatu wa mahakamani hapo. Kabla ya kuvamia meza ya mshtakiwa Nassar, mwanaume huyo aliomba kupewa “dakika tano ili afungiwe na shetani huyo” Jaji Janice Cunningham akasema hawezi kuruhusu jambo hilo.
Lakini Margraves aliendelea kusisitiza apewe dakika moja na kusababisha vicheko vya chini chini kutoka chumba cha mahakama. Nassar, aliyewahi kuwa Daktari wa mazoezi wa Timu ya Olympiki ya Marekani, alishahukumiwa miaka 175 jela wiki iliyopita baada ya kutolewa ushahidi wa takribani waathirika 160 waliofanyiwa vitendo vya udhalilishaji kingono.

Akiwakilisha hukumu hiyo, Jaji Rosemarie Aquilina alimwambia Nassar: ” wewe hustahili kuonekana tena nje ya jela.”
Waathirika wengi ni wale waliochukuliwa kwaajili ya kutibiwa naye katika Chuo Kikuu cha Jimbo la Michigan, alipokuwa akifanya kazi kama Daktari wa michezo.


 

Zitto Kabwe azitaka CCM, Chadema kusitisha kampeni

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameviomba vyama vya Chadema na CCM kusimamisha kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge na udiwani kwa siku tatu kuomboleza kifo cha mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru.

"Kingunge  amesaidia kuimarisha CCM na baadaye akasaidia Chadema. Sioni busara vyama kuendelea  na kampeni. Nawaomba wasitishe leo, kesho na Jumatatu mwanasiasa huyu akizikwa wataendelea," amesema Zitto leo Februari 3, 2018 akiwa katika msiba wa mwanasiasa huyo, nyumbani kwake Kijitonyama, Dar es Salaam.

Vyama takriban 12 vipo katika kampeni za ubunge jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam na Siha mkoani Kilimanjaro. Kampeni hizo zilianza Januari 21 na kutarajiwa kumalizika Februari 16. Uchaguzi katika majimbo hayo na Kata 10 utafanyika Februari 17, 2018.

Kingunge aliyekuwa kada wa CCM mwenye kadi namba nane, Oktoba 4, 2015 alitangaza kukihama chama hicho na kusema hatojiunga na chama chochote lakini mara kadhaa alionekana akipanda majukwaa ya upinzani kumnadi aliyekuwa mgombea urais wa Chadema na Ukawa, Edward Lowassa kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Mwanasiasa huyo alifariki dunia jana Februari 2, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), anatarajiwa kuzikwa Jumatatu Februari 5, 2018 katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Wakati Zitto akieleza hayo, Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais (Utumishi  na Utawala Bora ), George  Mkuchika amesema atamkumbuka Kingunge  kwa mengi.

Amesema alimfahamu Kingunge miaka ya 1970 wakati akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kwamba mwanasiasa huyo mkongwe alikuwa akienda kutoa mihadhara  wakati huo wakiwa wanachama wa Tanu.

“Kifo chake kimenistusha kutokana na mchango wake mkubwa wa kuunganisha vijana,” amesema Mkuchika.

Wastara kwenda India kesho kwa matibabu

Wastara Juma.
BAADA ya gazeti hili kuandika habari yake kwa mara ya kwanza akiomba msaada wa matibabu ya mguu wake, hatimaye staa wa filamu Bongo, Wastara Juma amekamilisha kiasi cha shilingi milioni 37 alizokuwa akihitaji na kesho (Jumapili) anatarajia kuondoka nchini kuelekea kwenye Hospitali ya Sefaree iliyopo India kwa matibabu.

Wastara alisema kuwa, hakutarajia muitikio mkubwa wa kuchangiwa fedha hizo na anawashukuru wote waliofanikisha kupatikana kwa msaada huo.

“Niwashukuru Watanzania wote kwa kunichangia, nimshukuru Rais Magufuli na mkewe mama Janeth lakini kwa kipekee kabisa naomba nilishukuru gazeti lenu (Risasi Jumamosi) kwa kuwafanya watu wengine wajue nina tatizo gani na nahitaji msaada, bila nyie huenda mpaka leo ningekuwa nalia kitandani, asanteni na Mungu awabariki,” alisema Wastara.


Wastara pia ameishukuru Global TV Online ambayo ilirusha sauti yake na video ikionesha jinsi alivyokuwa akipata maumivu.

#VPL MATOKEO Lipuli 0-2 Yanga Mbeya City 2-1Majimaji TZ Prison 2- 0 Njombe Mji

No automatic alt text available.

Patashika ya mzunguko wa pili wa Ligi kuu soka Tanzania bara kuanza kutimua vumbi leo mechi zote

No automatic alt text available.

RAIS MAGUFULI KUTUNUKU KAMISHENI MAAFISA WAPYA WA JWTZ:





 Rais Magufuli, kutunuku kamisheni maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Watakaotunukiwa kamisheni ni maafisa wapya wa Tanzania na kutoka nchi marafiki 197 waliopata mafunzo katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli mkoani Arusha.

 Rais Magufuli ameanza kwa kutoa zawadi kwa waliofanya vizuri zaidi katika mafunzo hayo. Miongoni mwao ni pamoja na mwanafunzi aliyefanya vizuri katika medani zote.
Akifuatiwa na aliyefanya vizuri darasa.
Aliyefanya vizuri zaidi katika wanafunzi wote.
Aliyefanya vizuri kwa wanafunzi wa kigeni, Mkundane Beka



 

 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya January 3

Uchimbaji mafuta ya Petroli mkoani Morogoro kuanza Septemba 2018

Serikali imesema mradi wa uchimbaji mafuta katika Kisima kilichoanishwa kuchimbwa kwenye eneo la kijiji cha Ipera Asilia, kwenye hifadhi tengefu ya bonde la Kilombero, mkoani Morogoro, unatarajiwa kuanza rasmi mwezi Septemba, 2018 ambapo kisima hicho kinakadiriwa kuwa na mafuta kuanzia lita milioni 180 hadi 200.

Akizungumza jana Februari 2, 2018 katika kipindi cha maswali na majibu kwenye kikao cha nne cha mkutano wa 10 wa Bunge mjini Dodoma, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kinachosubiriwa ni kibali kutoka Baraza la Mazingira nchini (NEMC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), ili uchimbaji huo uanze rasmi.

“Mkataba ulishasainiwa tangu mwaka 2012 kilihobaki ni utekelezaji wa uchimbaji na ugunduzi wa mafuta, mafuta yanayotarajiwa kuchimbwa kwenye eneo hilo yanafikia milionii 180 hadi 200, mtaji ni mkubwa na utakua na manufaa kwa wananchi wako na nchi kwa ujumla,” alisema na kuongeza.

“Kinachosubiriwa ni kibali cha mazingira kutoka NEMC na mamlaka ya TAWA, mwezi Julai mwaka huu tumehakikishiwa mkataba utapatikana na Septemba uchimbaji utaanza rasmi.”

Serikali kupitia shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) liliingia mkataba wa utafiti na uchimbaji wa gesi na uvunaji mafuta na Kampuni ya Mafuta na gesi ya Swala (Swala Oil), ambapo katika utekelezaji wa mkataba huo iligundulika kuwepo kwa wingi mafuta ya petrol na gesi katika vijiji vya Mtimbira.

Ijumaa, 2 Februari 2018

Makamu wa Rais alivyohudhuria msiba wa Kapteni Bomani


Leo February 2, 2018 Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amehudhuria msiba wa Rubani wa Ndege za Serikali, Marehemu Kapteni Dominic Bomani aliyefariki jana kwa ajali ya ndege kwenye uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume.