mwana wa liganga blog ni blog ya kutoa taarifa, matukio, yaliyotokea katika ulimwengu hususani katika nchi yaTanzania
blog hii inasimamiwa na mwandishi wa habari kitaaluma bwana Deus Thomas liganga.lengo ni kutoa taarifa kwa umma,kwa maendeleo ya taifa na Dunia kwa ujumla
kwa mawasiliano kuhusu mtangazo, habari, wasiliana nasi 0659944423,deusliganga@yahoo.com,mzeeliganga@gmail.com
Jumanne, 11 Septemba 2018
Mwili wa aliyekuwa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Kofi Annan umewasili Ghana kwa ajili ya maziko
Mwili wa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan,
ambaye alifariki mwezi uliopita, umewasili katika nchi aliyozaliwa,
Ghana.
Mwili
wake uliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kotoka International Airport
mjini Accra, ukisindikizwa na familia yake na maafisa wengine wa Umoja
wa Mataifa
Kulikuwa na hali ya maombolezowakati mwili wake
ukiwasili uwanjani hapo na kupokelewa na Rais wa Ghana Akufo Addo na
viongozi wa kimila na kwa heshima ya kijeshi.
Mwili wake umehifadhiwa katika Ukumbi wa Kimataifa wa mikutano wa Ghana, wakati ukisubiri kuzikwa. DAVOS-KLOSTERS/SWITZERLAND,
30JAN09 – Kofi Annan, Secretary-General, United Nations (1997-2006);
Member of the Foundation Board of the World Economic Forum; Co-Chair of
the World Economic Forum Annual Meeting 2009, captured during the
session ‘Fresh Solutions for Food Security’ at the Annual Meeting 2009
of the World Economic Forum in Davos, Switzerland, January 30, 2009. Copyright by World Economic Forum swiss-image.ch/Photo by Sebastian DerungsKofi
Annan alikuwa ni Katibu mkuu wa kwanza wa Umoja wa Mataifa, kutoka
katika eneo la kusini mwa jangwa la Sahara na kuleta mafanikio sio tu
katika bara la Afrika, lakini pia dunia nzima.
Chanzo BBC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni