Jumamosi, 2 Juni 2018

YANGA YAMNASA MBADALA WA DONALD NGOMA KUTOKA BENIN,


Wakati vuguvugu la usajili Bongo likiwa linaendelea, tetesi zinaeleza kuwa Yanga imemalizana na Mshambuliaji Mbenin, Marcellin Koukpo, aliyekuwa anakipiga katika klabu ya Buffles du Burgou nchini kwao.

Yanga ambayo usajili wake unaonekana kuwa wa kimyakimya haijaweza kuweka wazi kuhusiana na kumyaka mshambuliaji huyo ambaye inaelezwa amekuja kuchukua nafasi ya Donald Ngoma aliyetimkia Azam FC.

Taarifa zinaeleza kuwa Koukpo amesaini mkataba wa miaka miwili kuwatumia mabingwa hao wa historia katika Ligi Kuu Bara kwa kuutwaa mara 27.

Imeelezwa pia mchezaji huyo ataungana na kikosi cha Yanga nchini Kenya, tayari kwa michuano ya SportPesa Super Cup inayoanza kesho.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni