Jumatatu, 21 Mei 2018

wasanii wakubwa saidieni wasanii chipukizi kukuza muziki wetu Tanzania - H Mwana






msanii wa  muziki wa kizazi kipya na bongo muvi  khalfan Suba maarufu kama H mwana [Faba money] ametoa wito kwa wasanii wakubwa  wa bongofleva kusaidia wasanii chipukizi [maunderground]ili kukuza  muziki na filamu  hapa nchini .

akizungumza na mwandishi wa mwana wa liganga blogspot.com, H mwana amesema kuwa wasanii wakubwa nchini wanajisahau kusaidia wenzao wanao anza  muziki na  filamu kwani pasipokujua nao  wametokea chini na kuweza kufahamika kupitia  muziki na filamu.

msanii  huyo ambaye anatamba na nyimbo ya kisambari , sir angel, ambapo pia ameweza kucheza filamu be care ful with women  ambapo aliweza kushirikisha wakongwe wa filamu hapa nchini  kama rose ndauka,ben branco maarufu kama beni na  mzee magari, ameongeza kuwa Tanzania ina vipaji lukuki  ambavyo vikitumiwa ipasavyo serikali inaweza kunufaika  kama itatengeneza mazingira mazuri kwa wasanii.
''tanzania  tumejaliwa vipaji  lukuki  kama serikali  itatengeneza mazingira bora kwa wasanii wa muziki na filamu tungekuza uchumi  kupitia tasnia hii''anasema  H mwana.
 

 msanii  huyo ambaye maskani yake ni katika jimbo la mlimba  mkoani morogoro  anatoa wito kwa wadau na  kusaidi wasanii wa chipukizi.

kwa upande wa  maandalizi ya kazi zake mpya  msanii huyo amesema anajipanga kuachia kazi zake mpya kwa upande wa muziki na filamu .''mashabiki wangu  wakae mkao wakula kwani kuna filamu yangu mpya    na ngoma mpya  ambapo vitatoka hivi karibuni, kwasasa najiandaa kufanya uzinduzi wa kazi hizo '' alisema  msanii huyo.

 hapa  H  mwana  anatoa wito kwa wasanii kuungana na kusaidiana kufanikisha ndoto zao.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni