
Wataalamu nchini Marekani wameshangazwa na kiumbe mmoja mfano wa mbwa mwitu aliyeuawa na mkulima huko Montana.
Mkulima huyo karibu na mji wa Donton alimpiga risasi kiumbe huyo wiki iliyopita alipokaribia mifugo wake, kwa mujibu wa maafisa.
Baada ya kumchunguza kiumbe hiyo walisema huenda akawa ni mbwa mwitu kwa sababu meno yake ni mafupi na makucha ni makubwa sana.
"Hatujafahamu hasa huyu mnyama ni wa familia ipi hadi uchunguzi wa DNA ukamilike," msemaji wa shirika ya samaki na wanyamapori alisema.
Alisema itachukua hadi wiki moja kwa matokeo kujulikana, ambayo yatasaidia kumtambua kiumbe huyo.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni