Alhamisi, 15 Machi 2018

MESSI ATUPIA MBILI BARCELONA IKIITWANGA CHELSEA NA KUITUPA NJE LIGI YA MABINGWA

4A3287AA00000578-5501573-image-a-86_1521058410542
Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya iliendelea tena usiku wa jana ambapo mechi iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka Afrika na duniani wa ujumla kati ya  FC. Barcelona dhidi ya Chelsea kumalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa mabao 3-0.
Alikuwa ni Messi aliyeanza kucheka na nyavu dakika ya mapema zaidi, dakika ya 3 na baadaye Oeusman Dembele akafunga la pili dakika ya 20, kabla ya Messi kuongeza jingine la 3 kwenye dakika ya 63 kipindi cha pili.
Barcelona sasa inasonga mbele kwa jumla ya mabao 4-1 baada ya mechi ya awali kwenda sare ya 1-1 pale Stamford Biridge.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni