Zitto yupo katika ziara ya mikoa mbalimbali kwa ajili ya kukagua na kuimarisha uhai wa chama hicho.
Akizungumza na millardayo.com na AyoTV Katibu Kamati ya Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa ACT Wazalendo Ado Shaibu amesema mpaka sasa bado yupo anashikiliwa na Polisi hawajui ni kosa gani ambalo Zitto Kabwe limefanya akamatwe
Nae Wakili wa Zitto Kabwe, Emmanuel Lazarus Mvula amesema jalada la mashataka dhidi yake limefunguliwa katika kituo cha Polisi Mgeta.
“Hivi Sasa saa 3.30 usiku ndugu Zitto amechukuliwa na OC-CID na polisi wenye silaha anapelekwa Kituo cha Polisi cha Wilaya, cha Dakawa ili kuandika maelezo kwasababu hakuna umeme katika kituo cha Polisi Mgeta” -Zitto Kabwe
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni