Jumapili, 18 Februari 2018

SIMBA YAKWEA PIPA KWENDA DJIBOUTI

Image may contain: 2 people, people standing and outdoor





Wakati kikosi cha Simba kimekwea pipa kwenda Djibouti kuivaa Gendamarie katika mechi ya Kombe la Shirikisho, kiungo wake, Said Hamis Ndemla amekuwa kivutio kwa mashabiki wa soka waliokuwa eneo hilo.

Ndemla alionekana kuchangamkiwa na mashabiki wengi wakimuita jina lake na baada ya hapo wakaanza kujadili suala la yeye kuwa na uwezo mkubwa wa kupiga mashuti wakati ana umbo dogo.

"Anaonekana ni mdogo, lakini mikwaju yake hatari sana yule mtu aisee," alisema mmoja wa mashabiki na kuungwa mkono na wenzake.

Ndemla amekuwa na sifa ya kupiga mashuti makali kiasi cha kujijengea imani hata ya kupata namba katika kikosi chini ya Mfaransa, Pierre Lechantre.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni