Jumanne, 27 Februari 2018

KOCHA NDANDA AWAAMBIA YANGA KESHO LAZIMA WAPIGWE TU HAKUNA JINSI



 Kipute cha Ligi Kuu Tanzania Bara kinataraji kuendelea tena Jumatano ya kesho kwa mchezo mmoja kupigwa katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona, ambapo Ndanda itaikabili Yanga.

Kuelekea mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Ndanda, Mussa Mbaya, amewatambia Yanga kuwa kesho ni lazima waache alama 3 mkoani Mtwara.

Mbaya amesema anatambua kuwa Yanga wanafukuzana na Simba kuwania ubingwa wa Ligi, lakini wanachokiangalia wao ni ushindi pekee kwenye mchezo huo.

"Sisi tumejiandaa vema, na nawaambia mashabiki wetu wajiandae kupokea alama tatu muhimu, ushindi utakuwa kwetu bila shaka yoyote" amesema Mbaya.

Ndanda itakuwa mwenyeji wa pambano hilo ikicheza mchezo wa 19 sawa na Yanga, lakini utofauti upo katika msimamo ambapo Ndanda ina alama 18, nafasi ya 13 na Yanga 37, nafasi ya pili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni