Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Azam FC na Young
Africans uliopangwa kuchezwa saa 1 usiku sasa utachezwa saa 10 jioni
kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi.
Mchezo huo ambao Azam Fc
ndio wenyeji wa mchezo huo kwa ratiba ya Bodi ya Ligi ilitakiwa kuchezwa
saa 1 usiku ,kutokana na Ukubwa wa Mechi hiyo na Usalama zaidi mda
umesogezwa nyuma na mchezo huo utachezwa saa 10.00 jioni.
Viingilio kwenye mchezo huo ni shilingi elfu kumi(10,000) kwa Jukwaa
Kuu na shilingi elfu saba (7,000) kwa majukwaa ya kawaida.
Pia Waamuzi wa mchezo huo wote ni kutoka Jijini Dar es Salaam ambapo muamuzi wa kati ni Israel Nkongo akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Josephat Bulali na mwamuzi msaidizi namba mbili Soud Lila, mwamuzi wa akiba Elly Sasii wakati Kamishna wa mchezo huo ni Omar Abdulkadir
Pia Waamuzi wa mchezo huo wote ni kutoka Jijini Dar es Salaam ambapo muamuzi wa kati ni Israel Nkongo akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja Josephat Bulali na mwamuzi msaidizi namba mbili Soud Lila, mwamuzi wa akiba Elly Sasii wakati Kamishna wa mchezo huo ni Omar Abdulkadir
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni