Ligi Kuu soka Tanzania Bara inatarajia kuendelea wikendi hii kwa michezo mitano kuchezwa kwenye viwanja mbalimbali hapa nchini
ingida United ikiwa katika Uwanja wake wa Namfua itaikaribisha Yanga SC katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Kagera Sugar watakuwa wenyeji huko Bukoba katika dimba la Kaitaba watakapo wakaribisha Tanzania Prisons.
Njombe Mji wakiwa nyumbani katika dimba la Sabasaba Njombe watawakaribisha Mbao FC.
Azam FC itashuka katika Uwanja wa Azam Complex Jijini Dar es salaam kucheza na Ruvu Shooting.
Ndanda FC wakiwa mkoani Mtwara watashuka katika Uwanja wa Nangwanda kucheza na Mtibwa Sugar.
Na hapo keshokutwa siku ya Jumapili ya Novemba 5 timu ya Lipuli FC ikiwa katika Uwanja wake wa nyumbani wa Samora mkoani Iringa itashuka dimbani kumenyana na Mwadui FC wakati Mbeya City itakuwa Sokoine Mbeya kuwakabili vinara wa ligi klabu ya Simba.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni