
Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka miwili na miezi mitano amelazwa
hospitali ya wilaya Handeni baada ya kufanyiwa kitendo cha ukatili cha
ubakaji na kutelekezwa porini na aliyemfanyia kitendo hicho.
Akiongea kwa uchungu mama mzazi wa mtoto huyo amesema kuwa wakati
wanatoka shamba yeye na mumewe wakasikia sauti ya mtoto kutoka msitu wa
jirani na nyumbani kwao na wakahisi kuwa ni sauti ya mtoto wao na ndipo
wakafuatilia na kumkuta mtoto analia kwa uchungu.
Nae mganga wa zamu wa hospitali ya wilaya Handeni amesema kuwa baada ya
kumpokea mtoto huyo walimfanyia uchunguzi na kubaini kuwa amebakwa hali
iliyomsababishia michubuko huku baadhi ya wananchi walio ongea na ITV
wakitaka mhusika apewe adhabu kali.
Nae kamanda wa polisi mkoa wa Tanga amethibitisha kutoa kwa tukio hilo
na amesema kuwa tayari mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la polisi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni