Jumatano, 25 Oktoba 2017

John Bocco yupo fiti kuivaa Yanga Jumamosi


 MSHAMBULIAJI wa Simba, John Raphael Bocco yuko fiti kwa mchezo na mahasimu wa jadi, Yanga Jumamosi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam baada ya kupona maumivu ya mguu.

Mshambuliaji wa zamani wa Azam FC, jana na leo amefanya mazoezi kikamilifu katika kambi ya Zanzibar kujiandaa na mechi ya Jumamosi dhidi ya Yanga.

Pamoja na Bocco, mchezaji mwingine aliyekuwa majeruhi, kiungo Mohammed ‘Mo’ Ibrahim naye yuko fiti na anaendelea na mazoezi Zanzibar.

Katika kambi hiyo, Simba inawakosa kipa Said Mohammed ‘Ndunda’, mabeki Shomary Kapombe na Salim Mbonde ambao wote ni majeruhi wa muda mrefu.

Kapombe hajacheza kabisa tangu arejee Simba kutoka Azam FC kutokana na kuumia kwenye michuano ya Kombe la COSAFA nchini Afrika Kusini akiwa na timu ya taifa, Taifa Stars Julai mwaka huu.

Ndunda aliuami Agosti kwenye kambi ya mazoezi Zanzibar kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga uliochezwa Agosti 23, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Mbonde aliumia kwenye mechi dhidi ya timu yake ya zamani, Mtibwa Sugar Oktoba 15 Uwanja wa Uhuru.

Mbonde ambaye atakuwa nje hadi katkati ya Novemba, aliumia siku moja na Bocco, ambaye yeye alipewa mapumziko ya wiki moja tu, wakati Ndunda na Kapombe hawatarajiwi kabisa kucheza mwaka huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni