Jumatatu, 26 Juni 2017

Mashirika yanayowatetea wasichana wanaojifungua yaonywa Tanzania

Rais Magufuli alisema kuwa wasichana wajawazito hawawezi kurudi shuleni


Mashirika yasiyokuwa ya serikali nchini Tanzania yameonywa dhidi ya kuendesha kampeni kutaka wasichana walio na watoto kuruhusiwa kurudi shuleni.
Waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Nchemba, ametishia kuyapokonya vibali vya usajili mashirika hayo kwa mujibu wa gazeti la Citizen.


Hii ni baada ya Rais John Magufuli kuuambia mkutano wa hadhara kuwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania wasichana wajawazito hawewezi kurudi shuleni,
Magufuli alisema: "Baada ya kufanya hesabu kidogo, atakuwa akimuomba ruhusa mwalimu kuenda kumnyonyesha mtoto anayelia.

chanzo na bbc

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni