Rais Pierre Nkurunziza
Mabadiliko hayo ya katiba ni pamoja na kurefusha muhula wa Rais kutoka miaka mitano hadi saba na kwa mabadiliko hayo yatamfanya Rais Nkurunziza kugombea tena kipindi cha mihula mingine miwili baada ya awamu yake sasa kumalizika mwaka 2020.
Hata hivyo, Serikali ya Marekani kupitia kwa Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Heather Nauert imesema kuwa mchakato wa kura za maoni juu ya mabadiliko hayo ulikuwa na dosari nyingi na haukuwa wa uwazi.
“Mchakato wa kura za maoni ulikuwa na dosari ya kutokuwepo uwazi, kufungiwa kwa vyombo vya habari, na jaribio la kuwashinikiza wapiga kura yanakwenda kinyume na makubaliano ya msingi katika kuunda serikali ya umoja wa kitaifa uliofikiwa nchini Arusha,” amesema Bi. Nauert kwenye taarifa yake aliyoitoa jana kwa Vyombo vya Habari.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni