Kabla ya kufikia uamuzi huo, maaskofu hao waliwaomba radhi waathirika wa vitendo hivyo pamoja na kanisa kwa “makosa makubwa waliyoyatenda”.
Bado haijafahamika mara moja iwapo Papa amekubaliana na ombi hilo la kujiuzulu ama la.
Amekuwa katika kukosolewa nchini Chile kwa uamuzi wake wa kumteua askofu ambaye alishutumiwa na kamati ya makasisi kuhusika na kulinda vitendo vya udhalilishaji wa kingono nchini humo.
Alipofanya ziara nchini Chile, Papa aliuambia umma wa wakatoliki walifika kumlaki kuwa anajisikia “maumivu na aibu” juu ya kashfa hiyo iliyolikumba Kanisa la Katoliki nchini Chile.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni