Ijumaa, 16 Machi 2018

WADAU WA ELIMU RUKWA WAPINGA TAMKO LA RAIS:


Wadau wa elimu wa manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa wamekuwa na mtazamo tofauti juu ya agizo la Rais Magufuli kufuta michango kwa wanafunziwa shule za msingi na sekondari, huku miundombinu ya shule nyingi mkoani humo ikiwa si ya kuridhisha jambo lililosababisha wanafunzi zaidi ya 1553 kukosa nafasi ya kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu.
Wadau hao wamesema kuwa tamko la rais halikuzingatia Jografia ya maeneo ya pembezoni mwa nchi kama vile mkoa wa Rukwa. Walidai kuwa ili kuinua hadhi ya elimu ambayo imekuwa nyuma tangu uhuru, ushiriki wa wananchi hauepukiki.
“Ni kweli serikali imetoa zaidi ya bilioni moja kwa ajili ya maendeleo ya elimu katika manispaa yetu, lakini fedha hizi ni tone ukilinganisha na matatizo tuliyo nayo. Haziwezi kutatua kila changamoto tulizonazo. hivyo basi michango ya wadau na wazazi haiepukiki,” Zeno Nkoswe mdau wa elimu manispaa ya Sumbawanga


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni