Jumamosi, 17 Februari 2018

UJENZI UWANJA WA NDEGE SONGWE -


Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye ameiagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege TAA kumchukulia hatua za kisheria mkandarasi DP Shaprya kwa kushindwa kukamilisha ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja wa kimataifa wa Songwe licha ya kuomba kuongezewa muda.
January 31 mwaka huu ndio mkandarasi huyo alitakiwa kukabidhi jengo baada ya kumuahidi Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof Makame Mbarawa alipotembelea jengo hilo Novemba mwaka jana. Tayari bilioni tisa zimeshatolewa lakini hadi sasa kazi haijakamilika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni