
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebaini mambo matano baada ya
kumchunguza Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship
(FGBF), Zachary Kakobe, ikiwemo kukwepa kodi na kuhifadhi mabilioni ya
fedha katika majaba na ndoo.
Taarifa iliyotolewa leo Februari 20 na Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo,
Charles Kichere pia imesema Kakobe alimuandikia barua Rais John
Magufuli kutokana na matamshi yake kwamba ana fedha nyingi kuliko
Serikali, kumuomba radhi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni