Jumanne, 20 Februari 2018

TRA - Kanisa la Kakobe Linahifadhi Pesa Kwenye Ndoo








Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imebaini mambo matano baada ya kumchunguza Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship (FGBF), Zachary Kakobe, ikiwemo kukwepa kodi na kuhifadhi mabilioni ya fedha katika majaba na ndoo.
Taarifa iliyotolewa leo Februari 20 na Kamishna Mkuu wa mamlaka hiyo, Charles Kichere pia imesema Kakobe alimuandikia barua  Rais John Magufuli kutokana na matamshi yake kwamba ana fedha nyingi kuliko Serikali, kumuomba radhi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni