
Baadhi
ya watu wamekuwa wakidai Radio ni chombo cha habari kinachokufa ,
lakini ukweli ni kwamba Radio imezidi kushamiri na itaendelea kuwa
chombo muhimu cha mawasiliano katika jamii ndani na nje ya masuala ya
kibinadamu.
Kauli
hiyo imetolewa na afisa mkuu wa mawasiliano wa shirika la Umoja wa
Mataifa la uhamiaji IOM, bwana Mark Doyle , katika kuadhimisha siku ya
Radio hii leo mjini Geneva Uswis, ambako shirika hilo limeandaa shughuli
maalumu kwa ushirikiano na mtandao wa mawasiliano ya athari za majanga
(CDAC)
Hafla hiyo iliyopewa kichwa “Radio ni uti wa mgongo wa mafanikio katika mazingira ya sasa ya teknolojia ya mawasiliano” imejikita katika mambo mawili, mosi kutanabaisha uhusiano uliopo baina ya matumizi ya radio na afya katika jamii zilizoathirika na majanga, na pili ni jumukumu muhimu la radio kwa jamii zinazohama au kukimbia vita na majanga mengine.
Akitoa mfano amesema kwenye migogoro ya vita kama Somalia na Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, Radio imekuwa na mchango mkubwa katika kazi za IOM kufikisha msaada na kuwafikia wahitaji ambako vyombo vingine vya habari kama tlevision, magazeti au mtandao wa interneti haufiki.
Hafla hiyo iliyopewa kichwa “Radio ni uti wa mgongo wa mafanikio katika mazingira ya sasa ya teknolojia ya mawasiliano” imejikita katika mambo mawili, mosi kutanabaisha uhusiano uliopo baina ya matumizi ya radio na afya katika jamii zilizoathirika na majanga, na pili ni jumukumu muhimu la radio kwa jamii zinazohama au kukimbia vita na majanga mengine.
Akitoa mfano amesema kwenye migogoro ya vita kama Somalia na Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR, Radio imekuwa na mchango mkubwa katika kazi za IOM kufikisha msaada na kuwafikia wahitaji ambako vyombo vingine vya habari kama tlevision, magazeti au mtandao wa interneti haufiki.
Leo ni siku ya radio duniani,
ikitambua kuanzishwa kwa Radio ya Umoja wa Mataifa mwaka 1946. Shirika
la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO liliridhia
kuadhimishwa kwa siku hii wakati wa kikao cha bodi yake tendaji cha
tarehe 29 mwezi Septemba mwaka 2011.
Ikiwa
leo ni siku ya radio duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa Antonio
Guterres amesema licha ya maendeleo ya teknolojia, bado radio imesalia
chombo adhimu katika kuleta jamii pamoja na kuwezesha watu kufikia uwezo
wao wa juu zaidi kimaisha.
Katika ujumbe wake wa siku ya leo yenye maudhui redio na michezo, Bwana Guterres amesema
(Sauti ya Antonio Guterres)
“Katika zama za maendeleo makubwa zaidi ya mawasiliano, radio imebaki na uthabiti wake wa kuelimisha, kuburudisha, kuhabarisha na kuhamasisha. Inaweza kuunganisha na kujengea uwezo jamii na kuwapatia sauti watu wa wa pembezoni.”
Na katika michezo ameenda mbali na kutoa mfano akisema..
(Sauti ya Antonio Guterres)
“Mwaka huu mashindano ya olimpiki ya majira ya baridi yakiendelea, tunatambua njia mbalimbali ambazo kwao utangazaji wa michezo unaleta watu pamoja katika msisimko na mafanikio.”
Katika ujumbe wake wa siku ya leo yenye maudhui redio na michezo, Bwana Guterres amesema
(Sauti ya Antonio Guterres)
“Katika zama za maendeleo makubwa zaidi ya mawasiliano, radio imebaki na uthabiti wake wa kuelimisha, kuburudisha, kuhabarisha na kuhamasisha. Inaweza kuunganisha na kujengea uwezo jamii na kuwapatia sauti watu wa wa pembezoni.”
Na katika michezo ameenda mbali na kutoa mfano akisema..
(Sauti ya Antonio Guterres)
“Mwaka huu mashindano ya olimpiki ya majira ya baridi yakiendelea, tunatambua njia mbalimbali ambazo kwao utangazaji wa michezo unaleta watu pamoja katika msisimko na mafanikio.”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni