Ensayne Wayne (kushoto) akiwa na mdogo wake Drumma Boy (kulia)
Fox5 inaripoti kuwa tukio hilo lilitokea katika duka liitwalo “The House of Fresh” ambalo ni duka la nguo la Drumma Boy liliopo huko jijini Atlanta. Ensayne Wayne alipigwa risasi ya kifua baada ya kushiriki katika shambulio hilo la bunduki kwa sababu ambazo bado hazijajulikana. Ensayne alikuwa akibeba bunduki pia.
Hakuna risasi nyingine zilizoingia ndani ya duka na hakuna mtu mwingine aliyeumia katika tukio hilo. Mtuhumiwa huyo inasemekana kuwa aliondoka na gari lenye rangi ya silva, kwa mujibu wa polisi wa Atlanta ambao bado wanatafuta uchunguzi zaidi. Na wameeleza kuwa mtuhumiwa ni mwanamume mwenye rangi nyeusi.
Drumma Boy alithibitisha kifo kwa kutoa ujumbe kupitia mtandao wa Instagram huku akionyesha kumbukumbu za zamani za familia yao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni