Jumatano, 14 Februari 2018

Nyumba ya familia ya GUPTA yenye ukaribu na Rais Jacob Zuma yazingirwa na polisi

Members of the Hawks special police unit stand guard outside Gupta home


Watu watatu wamekamatwa baada ya nyumba ya familia ya Gupta yenye utata nchini Afrika Kusini kuvamiwa katika muendelezo wa uchunguzi dhidi ya familia hiyo inayodaiwa kuwa na ushawishi mkubwa kwa serikali.
Familia tajiri ya wazaliwa wa India ya Gupta imeshutumiwa kwa kutumia urafiki wao na Rais Zuma kwa manufaa binafsi na kibiashara.
Bwana Zuma na wakina Gupta wote wamekana shutuma hizo dhidi yao.
Kwa kiasi shinikizo kubwa la Zuma kujiuzulu linatokana na uhusiano wake na familia hiyo.
Anatarajiwa kuzungumza hivi karibuni kuhusu wito wa chama cha ANC wa kuondoka madarakani.
Cheo cha Zuma kama kiongozi wa chama kilichukuliwa na makamu wake, Cyril Ramaphosa, Disemba mwaka jana ,lakini hadi sasa amekataa wito wa chama kujiuzulu.


Afisa mmoja wa chama amesema alikuwa tayari kuachia ngazi ndani ya miezi mitatu hadi sita ijayo, lakini viongozi wa juu wanataka atoke mara moja.
Kiongozi huyo mwenye kashfa nyingi amekuwa madarakani tangu mwaka 2009.
 

Askari Polisi mjini Johannesburg nchini Afrika Kusini wameizingira nyumba ya familia ya kitajiri ya ‘Gupta’ ambayo ipo na mahusiano ya karibu na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma.
Picha inayohusiana
Rais Jacob Zuma akiwa na baadhi ya wanafamilia ya kifahari ya GUPTA.
Kwa mujibu wa mtandao wa Reuters umedai kuwa polisi wamezingira barabara zote zinazoingia kwenye eneo la nyumba za familia hiyo huku wakiwa na silaha nzito za kijeshi.
Msemaji wa jeshi la polisi mjini  Johannesburg, Hangwani Mulaudzi amethibitisha taarifa hiza lakini amekataa kutolea maelezo kwa nini nyumba hiyo ya kifahari imezingirwa na polisi.
Tangu mwaka 20015 familia ya Gupta imekuwa ikishutumiwa na viongozi wa upinzani nchini Afrika Kusini kuwa inahifadhi mali za wizi zinazoibwa serikalini na Rais Zuma.
Ulinzi huo umekuja katika kipindi hiki ambacho Chama cha ANC kwa sauti moja kimetoa tamko la kumshinikiza Rais Jacob Zuma kujiuzulu nafasi yake ya urais.
Jana chama hicho kilimpa masaa 48 Rais Jacob Zuma kujiuzulu urais huku mwenyewe akitaka apewe muda wa miezi mitatu hadi sita kuchukua uamuzi huo.
 annesburg Jumatano asubuhi. 
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni