Jumatano, 14 Februari 2018

MBUNGE WA ZAMANI MTEKETA AFANYIWA UPASUAJI LEO



 Mbunge wa zamani wa jimbo la kilombero  kupitia ccm  Abdul mteketa amefanyiwa upasuaji leo katika taasisi ya tiba  ya mifupa na mishipa ya fahamu muhimbili MOI  kutokana na tatizo la magoti linalomsumbua.


mkuu wa kitengo cha  mawasiliano ya umma na ustawi wa moi  almas juma amesema  mteketa alifikishwa hospital hiyo februari 11,2018 anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji leo februari 14 ,2018

''amefanyiwa  upasuaji anaendelea vizuri mengine kuhusu  ugonjwa  atawajulisha lakini kwasasa bado yupo chini ya uangalizi wa madaktari ''amesema jamaa



mbali na kuwa  mbunge wa jimbo la kilombero  , mteketa pia ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu  katika vilabu  vya  simba ,pan africa . hivi karibuni alikaririwa na vyombo vya habari akisema ameugua kwa muda mrefu tangu akiwa mbunge wa jimbo  la kilombero .

mbali na hilo mteketa amemshukuru rais magufuli kwakumsaidia matibabu  yake.








Hakuna maoni:

Chapisha Maoni