.jpg/image1170x530cropped.jpg)
Amkani
si shwari tena kwenye jimbo la Ituri nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo, DRC ambako raia wanakimbia mapigano kati ya jamii ya wahemba na
walendu. Safari sasa ni kuelekea Uganda kupitia ziwa Albert.
Mtumbwi ukitia nanga kwenye ufukwe wa ziwa Albert, kila mkimbizi na kirago chake anachoona ni muhimu hapa ugenini, wilaya ya Hoima, nchini Uganda.
Ingawa wamefika salama hapa, wakimbizi hawa wanaweka rehani maisha yao wakikimbia mapigano ya kikabila kwenye jimbo la Ituri nchini DR Congo.
Simulizi za walikotoka ni mbaya ikiwemo wengine kuuawa, na vijiji kuchomwa moto.
Lakini Anita Mave ambaye aliponea chupuchupu anasimulia alichoshuhudia..
Walioponea uhai wao baadhi yao wamebakwa au kutekwa nyara..
Na ndio maana kasi ya kukimbia ni kubwa na sasa wengine wanasubiri chombo kiwasili waweze kuvuka Ziwa Albert na kuingia Uganda miongoni mwano ni Jack Bandinga.
Kwa upande wa Uganda, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasema msaada zaidi unahitajika kwa wakimbizi kwani chini ya mwezi mmoja wakimbizi zaidi ya 22,000 kutoka DR Congo wamevuka na kuingia Uganda na tayari wanne wamekufa maji ziwani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni