Ijumaa, 16 Februari 2018

DKT. SLAA NA MWENZAKE WAAPISHWA:


Rais John Magufuli leo Februari, 16 amewaapisha mabalozi wawili aliowateua kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Nigeria na Sweden.
Mabalozi walioapishwa ni pamoja na Muhidin Ally Mboweto ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Dkt. Wilbrod Peter Slaa ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Sweden.
Uteuzi wa Mabalozi hao kuiwakilisha Tanzania katika nchi walizopangiwa umeanza jana Februari, 15.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni