Serikali imetoa tahadhari kuhusu ugonjwa wa homa ya Chikuganya ambao
umeripotiwa na vyombo vya habari kutokea jijini Mombasa nchini Kenya.
Taarifa iliyotolewa leo, Ijumaa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu imesema kuwa mpaka sasa Shirika
la Afya Duniani (WHO) bado halijatoa taarifa rasmi lakini kama nchi
wameona ni vyema wakatoa tahadhari ya kuzingatiwa kwa muingiliano mkubwa
wa watu baina ya nchi hizi mbili za Kenya na Tanzania.
Kwa mujibu wa Wizara ya Afya wanasema, ugonjwa wa Chikunganya
unasababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa na mbu aina ya Aedes na
kusema ugonjwa huo siyo mgeni nchini Tanzania kwani ulishawahi kutokea
katika maeneo ya kusini huko Makonde mpakani mwa Tanzania na Msumbiji.
Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari imezitaja baadhi ya dalili za wagonjwa huo kuwa ni pamoja na homa kali, kuumwa kichwa, maumivu ya kichwa na uchovu, kichefuchefu na kizunguzungu na wakati mwingine tumbo kuuma.

Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa kwenye vyombo vya habari imezitaja baadhi ya dalili za wagonjwa huo kuwa ni pamoja na homa kali, kuumwa kichwa, maumivu ya kichwa na uchovu, kichefuchefu na kizunguzungu na wakati mwingine tumbo kuuma.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni