TABORA JAZZ ‘Wana
Segere Matata’ ni bendi pekee ya muziki wa dansi inayojulikana huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo.
Kauli
hiyo nzito ilitolewa na mkongwe wa muziki wa dansi toka Jamhuri na Kidemokrasia ya Congo, Tabu Ley Rochereau.
Akiwa ziarani hapa Tanzania,
Tabu Ley aliwahi kufanya mkutano na waandishi wa
habari katika hoteli Kilimanjaro. Moja kati ya
maswali aliyoulizwa ni kutaka kufahamu ni bendi gani hapa Tanzania
wanayoijua huko kwao DRC. Tabu Ley pasipo kupepesa macho, alikiri kwa kujibu
kwamba ni Tabora Jazz pekee ndiyo
inayojulikana huko.
Tabora Jazz
ni bendi kongwe iliyoanzishwa mwaka 1954, ambao katika historia ya Tanzania
ndiyo mwaka ambao chama cha TANU kilianzishwa.
Bendi
hiyo ilikuwa ikiongozwa na waanzilishi
akina Hamis Ali Songo na Mlekwa
Selemani, ikiwa na makazi yake mjini Tabora ikipiga na kutoa burudani murua za muziki
wa dansi katika kumbi za Lumumba kwenye
kona ya mitaa ya Usagara na Rufita ambako ndiko yalikuwa makao makuu yake. Pia
walikuwa wakipiga katika Baa za Bizeta, Maua
na nje ya mji wakialikwa.
Miaka ya nyuma Tabora Jazz ilikuwa na upinzani mkubwa na
bendi ya Western Jazz ya jijini Dar es
Salaam. Upinzani huo ulijiri baada ya Bendi ya Western
Jazz kukwapua kwa nyakati tofauti nguli wawili toka Tabora Jazz., kwa ambao
walihamisha ‘melody’ yao
kuipeleka huko.
Wanamuziki hao walikuwa
akina Wema Abdallah na Rashidi Hanzuruni ambao walikuwa mahiri kwa
kulicharaza gitaa la solo,ambao walihamisha ‘melody’ kuzipeleka Western Jazz.
Nyimbo nyingi
za bendi hiyo zilipigwa mno katika kituo
cha Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na kusikika sehemu kubwa Afrika ya Mashariki na Kati.
Huko nchini
Rwanda kulikuwepo redio Rwanda
iliyokuwa na kipindi cha muziki nyakati za jioni kikiendeshwa na mtangazaji
Kabendera Shinani, ambaye alikuwa akizipiga nyimbo za Tabora Jazz kila mara.
Redio hiyo ilikuwa ikisikika hapa nchini maeneo mbalimbali ya mikoa ya Kigoma,
Tabora, Shinyanga, Mwanza na Kagera (Ziwa Magharibi) wakati huo.
‘Wana
Segere matata’ waliwika sana miongoni mwa bendi kubwa hapa nchini zikiwemo Morogoro
Jazz, Cuban Marimba, Western Jazz, NUTA Jazz, Dar. Jazz, Kilwa Jazz, Urafiki
Jazz, Jamhuri Jazz na nyingine nyingi.
Mji wa
Tabora wakati huo ulikuwa na ushindani mkubwa katika muziki kati ya Tabora Jazz
na bendi zingine zilizokuwepo wakati huo za Kiko Kids iliyokuwa ikiongozwa na
Salimu Zahoro na Nyanyembe Jazz iliyoibuka na kibao chake cha ‘Rangi ya Chungwa’
wimbo ambao hadi sasa bado unarindima kwenye vituo vingi vya redio na kumbi
nyingi za burudani hapa nchini.
Pia mji
wa Tabora enzi hizo kulikuwa na umkumbi mkubwa wa Disco uliokuwa ukijulikana
kwa jina la ‘Mwana Isungu’ uliokuwa ikiteka kundi kubwa la vijana wa mji huo kwa kuporomosha muziki
maridhawa, zikiwemo nyimbo za Tabora Jazz na Nyanyembe Jazz.
Kama
nilivyokudokeza hapo awali kwamba bendi hiyo ilianzaishwa kabla ya Tanganyika kupata Uhuru, hivyo
iliendeleza mfumo wa kikoloni. Mfano mmoja ni kwamba katika miaka ya 1960
ilikuwa ni marufuku kwa mpenzi au shabiki kuingia ukumbini kucheza muziki
pasipo ‘kunyonga’ Tai shingoni, licha ya pesa zake. Hii ilikuwa ni moja ya njia
ya kuzingatia utanashati na nidhamu kwa
ujumla.
Bendi
hiyo ilipiga katika mitindo ya Segere matata, Segua Segua, na Mambo
Milekana, ikiwazingua wapenzi wa muziki mjini humo.
Miaka hiyo Tabora Jazz alitoka na nyimbo
zao ngingi zikiwemo za Usijifanye mwewe, Mariam mpenzi, Zabibu No.2, Anna, Regina, Mambo
Mileka, Tucheza Segere, Dada Mwantumu, Serafina,Tamaa yako, Alhamdulilah,
Nashukuru sana, na Dada Asha.
Zingine
ni pamoja na Zabibu, Halima, Dada Helena, Lucie, Farida na Dada Mwantumu.
Kufuatia
ushindani mkubwa uliokuwepo mjini humo
kati yake na Nyanyembe Jazz na Kiko Kids, Tabora Jazz ilifumua vibao ingine
vikali vya Chakula kwa Jirani, Mapenzi
hayana mganga, Mambo Mileka, Ujana una mwisho. Salima, Dada Remmy, Tucheze
Segere na Rukia wajidanganya.
‘Segere
matata’ wakati huo ilikuwa na mashabiki waliokubuhu. Kwa wakazi wa Tabora mjini
hawawezi kumsahau shabiki mmoja aliyejulikana kwa jina la ‘Mzee Segua’ ambaye
alikuwa hakosi onyesho lolote la bendi hiyo akicheza ‘Segua Segua, mtindo
aliokuwa aikiumudu hadi kufikia kupachikwa jina la ‘Mzee Segua’
Alikuwa
ni Mzee mwenye vituko ukumbini, akiwa na mfanyakazi katika Ofisi moja ya serikali
mjini humo kama
dereva. ‘Mzee Segua kwa mapenzi yaliyopitiliza mbele ya tabora Jazz, alidiriki
kukakataa uhamisho kwenda Wilaya ya Urambo, akitoa sharti ili aende huko basi Bendi
hiyo nayo ihamishiwe Urambo. Yaelezwa kwamba baadaye alifukuzwa kazi.
Kikosi kamili cha wanamuziki waliokuwa wakiunda kikosi
kamili cha bendi hiyo kilikuwa cha akina Athumani Tembo kwa upande wa gitaa la
Soloakisaidiana na Shem Ibrahim Karenga
aliyekuwa akipiga gitaa la solo, akitunga na kuimba. Salumu Luzira alikuwa akiliungurumisha gitaa zito besi na ugeweza kulilingalinisha na alivyokuwa akipiga
Suleiman Mwanyiro ama Lofombo wa Empire
Bakuba.
Wengine katika safu hiyo walikuwa Kassim Kaluwona, aliyekuwa akilicharaza gitaa
la rhythm akisaidiana na Issa Ramadhani
‘Baba Isaya’ Waimbaji walikuwa ni akina Ramadhani
Hamis Nguligwa, Ismail Mwangoko, na Msafiri Haruob, ambaye baadaye alijiunga na Mwenge
Jazz ya Jijini Dar es Salaam.
Kuna
msemo wa waswahili usemao kwamba ‘ Vizuri huigwa na Vitamu huonjwa’ Msemo huo ulijidhihirisha wazi kwa Bendi
kubwa toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ya Soukos Stars, ambayo iliiba
nyimbo za Dada Asha wa Tabora Jazz na Vigeregere wa Western Jazz.
Kwa
umahiri mkubwa wa bendi hiyo ya Soukous
Stars ilitoka na mseto wa nyimbo nyingi zikiwemo za Dada Asha na
Vigeregere katika album moja ya ‘ Nairobi by Night’
Shem Karenga
alijaribu kufuatilia haki miliki yake
pasipo mafanikio kwa kuwa nchi yetu ilikuwa bado haijatunga sheria ya haki
miliki.
Tabora
Jazz iliposambaratika mwaka 1980, sanjari na Bendi za Nyanyembe Jazz na Kiko
Kids, nazo zilienda mrama na baadaye kuondoka katika taswira ya muziki hapa
nchini.
Kutoweka
kwa Bendi hizo kuliwaacha wapenzi wa muziki wa dansi wa mji huo ambao
waliupachika jina la ‘Mboka’ wakijawa na simanzi tele, licha ya kuanzishwa kwa
bendi nyingine ya Tabora Jazz ‘Sensema Malunde’ ambayo imeibuka miaka ya
karibuni ikiwapa burudani.
Bendi ya Tabora Jazz
ilikuwa na makazi yake mjini Tabora ikipiga muziki wake katika ukumbi wa
nyumbani wa Lumumba.
Nyimbo nyingi za bendi
hiyo zilipigwa mno kwenye kumbi za starehe pamoja na kituo cha Radio Tanzania
Dar es Salaam(RTD) na vituo vingine vya Radio vya Afrika ya mashariki.
Tabora Jazz ilitamba
kwa mitindo yake ya za Segere Matata, Segua Segua na Mambo Mileka.
Mji wa Tabora
unaelezwa kwamba ulianza kupata burudani za muziki wa dansi hata kabla ya
chama cha TANU hakichaanzishwa.
Kwa mujibu wa Hassan
Athuman ambaye aliyekuwa mwanamuziki wa enzi hizo akipiga gita la solo katika
bendi za Tabora Jazz, Kiko Kids, Nyanyembe Jazz na Milambo Jazz ‘Sona
Sona’ kwa nyakati tofauti.
Alisimulia kuwa
mnamo mwaka 1953 ilianzishwa bendi ya muziki wa dansi iliyopewa jina la Staff
Jazz ikiongozwa na Hamisi Wampa.
Vyombo vya muziki vya
bendi hiyo vilinunuliwa na mfadhili mmoja wa kabila la Kimmanda’ toka nchini
Malawi, aliyenunua vyombo hivyo wakati huo akiwa mfanyakazi wa Bomani.
Staff Jazz ilikuwa na
mdhamini akiitwa mwalimu Hasanari. Waanzilishi wake walikuwa akina Hamisi
Ali Songo ‘ngoma kubwa’ , Hamisi Ngege alikuwa mpiga ngoma ndogo, Dani
Kafumu na Nzige wapulizaji tarumbeta, Akbaru Hasanari Dremsi ‘ngoma
kubwa’ Joseph Kayombo ‘bambo’ mwimbaji, Moshi ‘marakasi’, Saidi ngoma
ndogo’ Haji Sungura ‘mlangoni’, Swedi Mandanda 1953/56/58 Hamisi Issa
‘’trarumbeta’ na ryhtm. Hii ilikuwa kati ya miaka ya 1953 hadi 1958.
Wanamuziki wengine
walikuwa akina Abdi Fundi upande wa ‘sax’ Athuman Tembo kuimba na ‘solo’
Zakaria Tenda wema(mwimbaji) Sylvester Chifunda ‘mwimbaji’ Juma Athumani
‘drums’ aka Juma Lumango na Mlekwa Suleimani mmoja wa viongozi. Rajabu Risasi
upande wa gita la besi.
Staff Jazz ilikuwa
ikipiga muziki kwenye ukumbi wa baa ya Rufita ambayo baadaye ukabadilishwa na
kuwa Lumumba uliyokuwa katika kona ya barabara za Rufita na Kapembe,
katikati ya mji wa Tabora.
Bendi hiyo kwa sababu
ambazo hazikuainishwa, mwaka 1954 ilisambaratika.
Busara na hekima za
Hamis Alli Songo zilimfanya aifufue bendi hiyo mwaka 1956 kwa jina lingine la
Tabora Jazz.
Yaelezwa kuwa Mlekwa
Selemani aliyekuwa shabiki mkubwa wa bendi ya Kiko Kids, akajiunga na Tabora
Jazz na kuwa mmoja wa viongozi wa bendi hiyo.
Mwaka 1958 bendi hiyo
ilichukuliwa kwenda Kanda ya Ziwa kwa ajili ya kuhamashisha nguvu ya chama cha
TANU wakiongozana na viongozi wake Rashid Mfaume Kawawa, Mzee
Herman Pacha, mama Mosi Tambwe na mumuwe Abdallah Selemani.
Bendi iliporudi
Rashidi Hazuruni mwaka 1959 aliondoka kwenda Dar es Salaam akajiunga na Quban
Branch iliyokuwa ikiongozwa na Mzee Mwaipungu.
Kati ya mwaka 1960 na
1961 bendi ilikuwa na wapigaji gita la solo wawili akina Abdi Fundi na Matata.
Mwaka uliofuatia Athumani Tembo akaongezeka katika ukung’utaji wa gita hilo.
‘Maisha ni kuhangaika’
usemi huu ulijionesha wakati Rashidi Hazuruni aliporejea tena kupiga muziki na
Tabora Jazz mwaka 1963.
Tabora Jazz ilisheheni
wanamuziki wengi wakiwemo akina Hamisi Wampa aliyekuwa Kiongozi, Hamisi Alli
Songo na Akbaru Hasanari Dremsi walikuwa wadunda ngoma kubwa, Mambosasa alikuwa
akipiga ukulele (gita la kizamani). Mambosasa ndiye aliyekuwa baba yake mzazi
na Athumani Mambosasa, aliyewahi kuwa mlinda mlango wa Klabu ya Simba.
Said na Hamis Ngege
walikuwa wakipiga ngoma ndogo, Dani Kafundu na Nzige walikuwa
wapulizaji wa tarumbeta wakati Joseph Kayombo ‘Bambo’ alikuwa mwimbaji.
Kwa upande wa marakasi
alikuwemo Moshi, Haji Sungura aliyekuwa mlinzi ‘mlangoni’, Swedi Mandanda
alikuwa mcharazaji wa gita la solo, Hamisi Issa alikuwa akipiga gita la kati
‘rhythm’ na Tarumbeta.
Wanamziki wengine
walikuwa Athumani Tembo kwenye solo, upande wa gita la rhythm walikuwa
Hamis Issa na Fundi Hassan Athumani.
Besi liliungurumishwa
na Kassim Mponda aliyeondoka katika bendi hiyo mwaka 1965 mwishoni, akifuatana
wanamuziki wengine akina Rashidi Hazuruni na Omari Kayanda wakaenda kujiunga na
Western Jazz.
Mwaka 1966 Tabora Jazz
ikapata mpiga solo mwingine aliyejulikana kwa jina la Stan kuziba pengo la
Rashidi Hanzuruni.
Upande wa safu ya
waimbaji walikuwa Atrhumani Tembo, Omari Kayanda , Sylvester Chifunda na Joseph
Kayombo ‘Bambo’
Mpigaji bongos (ngoma
ndogo) alikuwa Juma Athumani ‘kisegeju’ Abdi Fundi alikuwa akipuliza saxophone
’mdomo wa bata’
Kati ya mwaka 1964 na
1965, Tabora Jazz walirekodi nyimbo baadhi yake zikiwa za Ndugu sikilizeni,
Tuambie, Dunia haina mwisho, Mwanawanyeje na nyinginezo.
Mwaka 1967 Kassimu
Kaluwona alikwenda Kigoma na kuweza kuwaleta Wema Abdallah, Hamis
Kitambi, Issa Ramadhani ‘ ‘Baba Watoto’ Mabrushi
Ramadhani
Mgoligwa na Hamisi Mkongo.
Mwaka 1968 Salumu
Luzira akaijunga na Tabora Jazz akitokea Nzega.
Mwaka 1971 Wema
Abdallah akaondoka Tabora Jazz akaenda Western Jazz, nafasi yake ikachukuliwa
na mpiga solo mwingine aliyejulikana ka jina la Kalii, alikitokea Kigoma Jazz.
Kwa kipindi kifupi
Said Mabera na Hassan Rehan Bichuka nao walijiunga na Tabora Jazz wakitokea
Rumonge Jazz.
Shem Karenga aliletwa
na Kassim Kaluwona toka Kigoma, kuja Tabora kujiunga na bendi hiyo Aprili 1972.
Shem baada ya kutua, alishiriki vilivyo katika
utengenezaji wa wimbo wa Dada Asha ambao baadaye
Wimbo wa Dada Asha
uliibwa na bendi ya Sokous Stars ya akina Lokassa ya Mbongo ya nchini Kongo na
kuichakachua ukiwemo wimbo wa Vigeregere uliopigwa na Western Jazz. Pia
mwanamuziki Lita Bembo na vijana
wake wa Stukas nao walikwapua na kuupiga wimbo huo.
Kwa mujibu wa Hassan
Athumani amsema kuwa wimbo wa Dada Asha, mtunzi wake alikuwa askari jeshi
aliyeomba atengenezewe wimbo huo.
Tabu Ley aliiona album
yenye wimbo huo wa Dada Asha akiwa Nairobi na aliinunua akaenda kuiuza nchini
Kongo, Poland na Ubelgiji.
Bendi hiyo baadaye
akajipanga upya kwa kupata damu changa ili kuendeleza muziki wake.
Iliongeza watunzi na
waimbaji wengi akiwemo Msafiri Horoub, Madaraka Morris, Ismail Wangoko na
wengine wengi.
Kwa umoja wao
wakafyatua nyimbo nyingi zilizoweza kuridhisha nyoyo za wapenzi na mashabiki wa
Tabora Jazz. Nyimbo hizo ni Ashura, Helena, Mapenzi ulimi, Visa uache, Lucie
umeniacha, Zabibun na Niambie leo Kaka. Ziningine zilikuwa za Usijifanye Mwewe,
Mariam mpenzi, Zabibu No.2, Sofia mpenzi, Tatu, Serafina, Tamaa yako
na Asha No. 1. Zote hizo zilikuwa zikitamba mno wakati huo. Zingine
ni pamoja na Alhamdulilah, Nashukuru sana, na Dada Asha.
Nyingine ni pamoja na Dada Mwantumu, Ujana una
mwisho, mwisho wake ni uzee. Zingine zilikuwa za Salima, Mapenzi Ulimi, Dada
Remmy na Rukia wajidanganya.
Wanamuziki wengi wanatajwa katika bendi hii ya
Tabora Jazz, baadhi yao wapo hai kama vile Shem Karenga, Ramadhani Mwanangwa
(rhythm) Salumu Luzira na wengine wengi.
Baadhi ya wanamuziki wanaotajwa katika makala
hii wamekwishafariki.
Walio haihaajishughulishi tena na maswala ya
muziki kufuatia umri kuwatupa mkono.
Bendi ya Tabora Jazz
haipo tena katika ulimwengu wa muziki.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni