bbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbbb
Franco ambaye alizaliwa Tarehe 6 Julai,
1938, katika Kijiji cha Sona Bata Magharibi ya Kongo, atakumbukwa na watanzania
wakati alipofanya onyesho kweye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mwaka 1973.
Baba yake Joseph Emogo alikuwa
mfanyakazi wa Shirika la reli wakati mama yake alikuwa mama wa nyumbani akioka
mikate na kuuza Sokoni wakati akiwa bado mdogo wazazi wake walihamia katika
Jiji la Kinshasa.
.
Franco alipofikisha umri wa miaka Saba alitengeneza gitaa la kienyeji ambalo alilitumia
kupiga na akiwavutia wateja pembeni mwa
mama yake wakati akiuza mikate.
Kipaji chake kiligunduliwa na mpiga gita
Paul Ebengo Dewayon ambaye alijitolea kumfunza Franco jinsi ya kupiga vyema Ala hiyo.
Mwaka 1950, wakati huo akiwa na umri wa
miaka 12, alitengeneza jina akiwa katika bendi ya Watam ya Ebengo Dewayon ambaye
alikuwa kiongozi wa bendi hiyo.
Alizikonga nyoyo za wapenzi kwa uwezo wakemkubwa wa kupiga gita ambalo
lilikuwa kubwa kuliko yeye.Miaka mitatu baadaye Franco alirekodi wimbo wake wa kwanza uliokuwa na jina la
Bolingo na Ngai na Beatrice.(mpenzi wangu Beatrice) baada ya kukubalika kuwa mmoja
wa wana bendi ya Loningisa Studio, kiongozi wa bendi hiyo Henri Bowane alitoa
nadhiri kwamba ataishi na Franco katika maisha yake yote yaliyosalia.
Chini ya Henri Bowane Franco akawa mpiga
gita la solo ambapo alikuwa kipiga staili ya Sebene na akaanza kutunga na kuimba yeye mwenyewe
kwa staili za rumba na za kiafrika na hata za kilatini.
Mwaka 1955 pamoja na kwamba alikuwa
akipewa kazi nyingi katika Studio hapo Franco aliunda bendi akiwa na Jean Serge
Essous iliyokuwa ikipigia katika Baa ya Ok.
Huko Kinshasa.
Mwaka uliofuatia bendi hiyo
ilibadilishwa jina na kuwa Ok Jazz na baadaye ikaitwa T.P.Ok. Jazz kuenzi
sehemu ilipoanzia bendi hiyo yaani katika Bar yenye jila la OK (OK. Bar)
Katika kipindi cha mwaka mmoja bendi
yake ya T.P.Ok Jazz ikagundulika kwamba inataka kumpiku Vicky Longomba ambaye
alikuwa katika bendi ya Grand Kale ya African Jazz ambayo ndiyo ilikuwa bendi
kubwa nchini Kongo.
Franco alishadai kwamba bendi yake ya Ok.Jazz
ilitoa zaidi ya album 150 katika kipindi cha miaka 30.
Mwaka 1958 Franco alifungwa kwa kosa la ajali ya barabarani.
Purukushani za kisiasa katika nchi yake
ya Kongo Franco alilazimika kuhamia Ubelgiji kwa ajili ya kurekodi nyimbo zake.
Baada ya nchi kutulia ikiwa chini ya
uongozi wa rais Mobutu Seseseko Kuku Ng’endu Wazabanga ambaye alibadilisha jina
la Kongo kuwa Zaire, Franco alirudi nchini mwake na kafanya tamasha kambambe la
Festival Ok. Jazz f African Arts lililofanyika Kinshasa mwaka 1966.
Ok Jazz iliisaidia sana Serikali ya Mobutu katika mambo ya
kisiasa kupitia nyimbo zake zilizokuwa na mafunzo mengi.Franco hakuona soni
katika kusifia mazuri wala kuonya mabaya pamoja na kwamba aliwekwa lupango mara
nyingi alipokiuka taratibu za nchi.
Mwaka
1970 Franco alipata pigo kubwa kwa kufiwa na mdogo wake Bavon Marie Marie amabaye kifo chake
kilitokana na ajali ya gari alipokuwa akiendesha kwa hasira baada ya
kukorofishana na kaka yake Franco juu ya mwanamke ambaye pia alikufa katika
ajali hiyo.
Mwaka
1980 Serikali ya Kongo (Zaire)
ilimtunuka hadhi ya kuwa Babu wa muziki wa Kongo kama
heshima kwa juhudi zake za kufufua uchumi amabo ulikuwa ukiyumba nchini humo.
Wakati wa maisha yake aliwahi kuongeza
uzito ghafla na kufikia paundi 300 ambazo ni sawa na kilo 136.
Franco alifyatua wimbo mkali mwaka 1985,
uliotikisa nchi wa Mario. Lakini mwaka 1987 fununu zikaanza kuzagaa kwamba Franco
yu mgonjwa.
Wimbo aliotengeneza mwaka huo kabla ya
kifo chake ulikuwa wa ‘Attention na SIDA’(Jihadhari kwa Ukimwi / AIDS)
Franco alifariki tarehe 12, Oktoba 1989
akiwa katika hospitali mojawapo huko Ubelgiji na mwili wake ulisafirishwa
kupelekwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (Zaire zamani) ambako jeneza lake
lilipitishwa mitaani kuagwa na wananchi likisindikizwa na ulinzi mkali wa
Polisi na baadaye serikali ikatangaza siku nne za maombolezo ya kitaifa.
Wakati wa siku hizo za maombolezo radio
ya taifa hilo ilikuwa ikipiga nyimbo za Franco hadi tarehe 17, Oktoba 1989 alipozikwa kwa heshima zote za kitaifa.
TUMKUMBUKE GRAND MAITRE LUAMBO MAKIADI / NYIMBO ZAKE ZILIZO PIGWA MARUFUKU
Miaka 25 Sasa tokea Afariki Dunia Guiji wa Muziki wa Rumba FRANCO LUAMBO MAKIADI.
Ingawa Mengi yamesha andikwa kwa kumhenzi GRAND MAITRE FRANCO, Leo hii nachukua fursa ya kuchambua Baadhi ya Nyimbo zake zilizo pigwa Marufuku.
Wala sio Siri tunapo tamka ya kwamba ” GRAND MAITRE LUAMBO MAKIADI FRANCO ” katokea kua Tajiri sana katika kipindi cha Utawala wa Rais MOBUTU SESESEKO.
Mbali na Urafiki ambao FRANCO LUAMBO alikuanao na RAIS MOBUTU, ilifikia wakati fulani Serekali ikazipiga marufuku Baadhi ya Nyimbo zake zilizo kua na Ujumbe uliokeuka Maadili ya Umma.
Kutokana pia na Sababu mbali mbali, SEREKALI YA RAIS MOBUTU, ilikua makini sana na Wanamuziki, hasa palikua na Watu hodari ambao kazi yao kuu ilikua kufanya uchunguzi wakina kwa Ujumbe unao patikana kwenye NYIMBO. Ikiwa kwa Namna moja au Nyingine kwenye Wimbo wewe Msanii ukithubutu Kutamka Jina la Mpinzani, Basi Wimbo huo kamwe hauta ruhusiwa na Wewe mwenyewe utajikuta ukiwa matatani.
1. Mkasa kama huo umemkuta TABU LEY ROCHEREAU, wakati katunga Wimbo ” KASHAMA NKOYI ” kwenye Wimbo huo, ROCHEREAU kayatamka Maneno haya : ” Boni Oweleli, Okende liboso ya Baninga, Soki okutani na LUMUMBA okoloba nini PAPA ? Tokengelaki yoo te KASHAMA NKOYI / INAKUAJE UKASAFIRI, WATUTANGULIA SISI WENZIO, HUKO UENDAKO, UTAKAPO KUTANA NA LUMUMBA UTAMWAMBIAJE BABA ? WALA HATUJAWAHI KUFANYA UCHUNGUZI WA KINA KWA YALE YALIYO KUKUTA ” KASHAMA NKOYI “.
Wimbo umepigwa Marufuku, sio kwasababu Katajwa LUMUMBA hapana, Bali Jina ” KASHAMA NKOYI “, Serekali ya MOBUTU yamushutumu ROCHEREAU TABU LEY kutumia Jina hilo Bandia kwakumhenzi ” PIERRE MULELE ” ambae alikua Mmoja kati ya MAWAZIRI wa EMERY PATRICE LUMUMBA,SHUJAA WA UHURU WA CONGO. Baada ya kuuwawa LUMUMBA, PIERRE MULELE kasimama kidete kupambana na SEREKALI ya MOBUTU. Vikosi vya Waasi vilio tawala mashariki mwa Congo hasa kwenye Mikoa ya KIVU. VIlikua vikimchukulia yeye kama Kiongozi wao Mkuu. Ndiko katokea LAURENT DESIRE KABILA. PIERRE MULELE kauwawa Mwaka 1968.
2. FRANCO LUAMBO NA WIMBO WAKE ” LUVUMBU NDOKI “, Kwenye Wimbo huo, FRANCO kaimba kwa KIKONGO, Lugha yake ya Asili. Ujumbe kwenye Wimbo huo ni kwamba ” WEWE LUVUMBU MTU AMBAE KIJIJI KIZIMA KINAKUTEGEMEA, WANAKIJIJI WOTE WAKO CHINI YA USIMAMIZI WAKO, KUTOKANA NA UCHAWI WAKO, UMEWAMALIZA NDUGU ZAKO WOTE WAKIKE KAMAVILE WAKIUME, SASA WAKATI UTAKAPO FARIKI, NANI YULE ATAKAE KUZIKA ? MIMI FRANÇOIS NASHINDWA KABISA KULIA, KWAKWELI HUA NAJIULIZA, KWANI UCHAWI WAKO UPO MGONGONI AU TUMBONI MWAKO.
Wimbo huo Ulipigwa marufuku paletuu ulipo tolewa, SEREKALI ya RAIS MOBUTU, yasema kwamba, Kupitia Wimbo huo, FRANCO LUAMBO MAKIADI kawatukuza Wanasiasa Wanne Walio Uwawa kwa Kunyongwa kwa Madai kwamba walikua na nia ya kuipindua Serekali Mwaka 1966. Wanasiasa hao walio nyongwa ni hawa :
1. JÉRÔME ANANY ( WAZIRI WA ZAMANI WA ULINZI WA TAIFA )
2. EMMANUEL BAMBA ( SENETA )
3. ÉVARISTE KIMBA ( WAZIRI MKUU WA ZAMANI )
4. ALEXANDRE MAHAMBA ( WAZIRI WA ARDHI )
Baada ya Wimbo huo kutolewa, FRANCO LUAMBO Tetesi zilimjia kana kwamba SEREKALI ipo kwenye harakati ya kumfungulia Mashitaka na Kumuweka Jela. LUAMBO kavuka yeye pamoja na Group lake nakwenda kujihifadhi kwa Mda JIJINI BRAZZAVILLE.
Akiwa JIJINI BRAZZAVILLE, RAIS MOBUTU kamtumia Wajumbe na kumshawishi arudi KINSHASA, maisha yake haitakua hatarini. FRANCO LUAMBO kaupokea wito huo ila kawa katika hali ya Mtu mwenye Kusita. Mwishowe kaamua kurudi KINSHASA.
Akiwa JIJINI KINSHASA, FRANCO LUAMBO kajikuta yuko matatani, Kakaribishwa na kikosi cha Wanajeshi. Wakamuamuru yeye na Group lake wapande ndani ya Gari lao, nakupelekwa moja kwa moja Jela ya NDOLO. Huko walikaa kwa Mda wa Siku Mbili, yasemekana Walicharazwa bakora sawasawa,
Baada yakutolewa kwenye Jela ya NDOLO, FRANCO LUAMBO na Group lake, wakahamishwa kwenye Kambi ya Jeshi ” TSHATSHI “. Huko pia wakashikiliwa kwa siku kadhaa wakiwa kambini humo.
Ndipo Ikatokea Siku amabayo RAIS MOBUTU akaja mwenyewe kujadiliana na LUAMBO MAKIADI. kamtamkia Maneno haya : ( KUANZIA LEO HII HADI ITAKAPO FIKIA WAKATI WA MIMI KUONDOKA MADARAKANI, UTAKUA UKINIIMBIA MIMI, WATAKIWA KUNIFANYIA KAZI ZANGU ZOTE, NA TENA KWA WAKATI WOWOTE NTAKAO KUHITAJI ) .
Nakwakeli Tokea siku hiyo, FRANCO LUAMBO kawa kiungo kikuu sana kwa Kampeni ya RAIS MOBUTU. na kutokana na ushirikiano huo, kanufaika sana kuwazidi Wanamuziki wengine wote wa Inchi hiyo katika kipindi hicho cha utawala wa Serekali ya MOBUTU SESESEKO KUKU NGBWENDU WAZABANGA JOSEPH DESIRE.
Mwaka 1978, FRANCO LUAMBO MAKIADI kawekwa tena JELA kutokana na Utunzi wa Nyimbo ( HELEINI na JACKIE ),
Nyimbo mbili hizo zilikua na Maneno machafu sana tena yaku yaharibu maadili ya Umma. Sheria ikachukuliwa kuzipiga Marufuku zisipitishwe kwenye Radio na TV ya taifa. FRANCO mwenyewe kajitetea, kasema wala NYIMBO hizo hajizauzwa Sokoni zilikua bado hazijawekwa kwenye CD. bali Watu walikua wakizisikiliza Wakati wa SHOO kwenye Ukumbi wake wa 1.2.3 KINSHASA.
Aliekua MWANASHERIA MKUU WA SEREKALI kipindi hicho ” Mr LEON KENGO WA DONDO “,kalisimamia swala hilo, nakuamuru FRANCO LUAMBO awekwe Jela, kapelekwa kwenye JELA ya ” LUZUBU ” inayo patikana kwenye MKOA WA BAS CONGO aliko zaliwa FRANCO.
Huko JELA, FRANCO kawa mwenye masikitiko, Kwanini RAIS MOBUTU kashindwa kumsaidia ? yeye ambae alikua akimchukulia kama Rafiki. FRANCO kapigwa na Ugonjwa wa HEMORRHOID. katabaanika kabisa. Kabaki na chuki na kinyongo dhidi ya MWANASHERIA ” LEON KENGO WA DONDO ” aliempeleka JELA. Haelewi kwanini kawekwa kizuizini wakati Hajawahi kuzidumbwiza Nyimbo hizo hadharani.
Miaka michache baadae, palitokea na mabadiliko kwenye Baraza la Mawaziri, LEON KENGO WA DONDO Kanenguliwa Cheo cha MWANA SHERIA MKUU WA SEREKALI na kutomwa JIJINI BRUSSELS kama BALOZI WA CONGO.
Furaha ilikuaje kwa FRANCO LUAMBO MAKIADI ?, bila kukawia kamtungia Wimbo ” TAILLEUR ” kwenye Wimbo huo FRANCO kanena haya : ( LIKAMBO NALOBAKI LOBI, MONOKO NA NGAI NGANGA / UTABIRI WANGU WATOKEA KUA KWELI, MDOMO WANGU KAMA WA MGANGA WA JADI ).
MOKOLO TONGA ABOTOLI TONGA OKOTONGA NANI ? / MWENYE SINDANO YAKE KESHA ICHUKUA, SASA UTATUMIA NINI ILIUENDELEE KUWACHOMA WENGINE?
OLOBAKI TROP NA ESIKA YANGOO BATIE YO PEMBENI LOBA LISUSU MAMA / ULIKUA UKIKIJIVUNIA SANA CHEO HICHO, SIUMEONA WAMEKUONDOA, UNANINI CHAKUONGEA? Wimbo huo pia ukapigwa Marufuku kwa Mda.
Mwaka 1982, RAIS MOBUTU Kamwitisha LEON KENGO WA DONDO , na kamteua kama WAZIRI MKUU WA INCHI.
FRANCO LUAMBO hajaridhishwa ni kitendo cha RAIS MOBUTU kumpa KENGO WA DONDO cheo cha WAZIRI MKUU, bila kusita Katunga Wimbo ” TRES FACHE “. Mtamsikia akiiimba : ( OKOSI NGAI MAMA YONAYE BOBOYANA, LOBI LISUSU BAKUTI YO NA VOITURE NA YEE, ELOKO NASALA NAYEBI TEEOO MOKILI / WANIDANGANYA KAMA NYIE WAWILI SIO TENA MARAFIKI, KESHO YAKE WATU WAMEWAONA MKIWA PAMOJA NDANI YA GARI, JAMANI KOSA GANI NILILOLIFANYA MIE!!! ). Kadhalika Wimbo huo Ulipigwa pia Marufuku.
GRAND MAITRE LUAMBO MAKIADI KAFARIKI DUNIA INCHINI BELGIUM TAREHE 12-10-1989.
SIKU YA MAZISHI YAKE, LEON KENGO WA DONDO AMBAE NDIE ALIEKUA WAZIRI MKUU, KAJA KUTOA HESHIMA ZAKE ZA MWISHO KWA NIABA YA SEREKALI.
WAKATI WA MISA YA MAZISHI YAKE, PADRE KASEMA : ” LUAMBO ALIKUA MTUME WA MUZIKI, HAKUNA ALICHOKISAHAU KATIKA UTUNZI WAKE, KAVICHAMBUA VITU KADHALIKA NA WATU WAKILA RIKA, HATA RAIS MOBUTU HAJAACHWA NYUMA.
NYIMBO ZAKE KADHAA ZILIPIGWA MARUFUKU, HATA HIVYO ZILIENDELEA KUPENDWA SANA NA UMMA. HUKU NYIMBO ZAKE NYINGINE HADI LEO HUCHUKULIWA KAMA NEMBO YA TAIFA.
mengineyo kumuhusu franco
MIAKA 25 iliyopita, Alhamisi ya
tarehe kama ya leo (yaani Oktoba 12, 1989) majira ya saa 1 asubuhi ndipo
niliposikia taarifa kupitia BBC kwamba mwanamuziki nguli wa rhumba barani
Afrika, Franco, alikuwa amefariki dunia.
Franco alifariki
wakati akitibiwa katika hospitali moja jijini Brusells, Ubelgiji, tena
alifariki mbele ya dada yake Marie Louise, mkewe Annie baadhi ya wanawe na baadhi ya
wanamuziki wa bendi yake.
Zile fununu zilizokuwa zimeenea tangu
mwaka 1987 kwamba nguli huyo alikuwa anaumwa sasa zikachukua sura mpya baada ya
watu kuanza kuvumisha kwamba huenda maradhi ya Ukimwi ndiyo yaliyokuwa
yamekatisha uhai wake.
Hii ilitokana na sababu mbili:
kwanza, tangu mwaka 1987 zilipovuma habari hizo kwamba jamaa anaumwa baadaye
akaanza kutoonekana mara kwa mara jukwaani. Lakini pili ni baada ya kutoa albam
yake – ya mwisho akiwa hai – ya Attention
na SIDA (Jihadhari na Ukimwi) mwaka 1987 ambayo kwa hakika hata taasisi za
afya za kimataifa, hususan zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi,
zinastahili kumuenzi hata leo.
Siyo ajabu kutokea kwa madai hayo,
kwa sababu siri ya mgonjwa anaijua mgonjwa mwenyewe na daktari, labda wawili
hao waamue kuitoa hadharani. Lakini ni jambo la kawaida hata sasa kwa binadamu
kujifanya madaktari – mabingwa wa kupima homa kwa viganja – ambapo wakimuona
mtu kakonda kidogo utawasikia wakisema “Yule, aah tayari ana ngwengwe!”
Franco mwenyewe katika kibao cha Attention na SIDA anaimba hivi: “Moto azua malade balobi Sida, moto azua fevre
balobi Sida, moto akonda balobi Sida, moto akufa balobi akufi na Sida…” (Mtu
akiugua wanasema anaumwa Ukimwi, Mtu akiwa na homa wanasema Ukimwi, mtu
akikonda tu wanasema ana Ukimwi, Mtu akifa wanasema amekufa kwa Ukimwi). Upo
hapo mjomba!?
Kwa vyovyote vile, dunia ilikuwa
imempoteza mwanamuziki ambaye alileta mabadiliko makubwa ya muziki wa Afrika
ukakubalika ulimwenguni kote.
Watanzania, hasa wale vijana wa
zamani, watamkumbuka kutokana na onyesho kubwa alilolifanya pale kwenye Uwanja
wa Taifa (Shamba la Bibi) jijini Dar es Salaam mwaka 1973.
Alipozaliwa Julai 6, 1938 katika
Kijiji cha Sona Bata, katika Jimbo la Bas Congo magharibi mwa Congo, si baba
yake Joseph Emogo wala mama yake …. waliojua kama mtoto huyo aliyezaliwa njiti
angeweza kuja kuwa mtu mashuhuri sana duniani.
Baba yake alikuwa mfanyakazi wa
Shirika la Reli enzi hizo za ukoloni wa Mbelgiji wakati mama yake alikuwa
akioka mikate
na kuiuza sokoni. Mama yake alimpa jina la Makiadi, lakini alipobatizwa
kanisani akapewa jina la Francis (ambalo ndilo Franco).
Wakati akiwa mdogo, wazazi wake
wakahamia jijini Kinshasa.
Akiwa
na umri wa miaka saba tu, Franco alitengeneza gitaa la kienyeji ambalo
alilitumia kupiga na kuwavutia wateja pembeni mwa mama yake wakati akiuza
mikate na maandazi.
Kipaji
chake kiligunduliwa na mpiga gita mashuhuri wa enzi hizo, Paul Ebengo Dewayon,
ambaye alijitolea kumfunza Franco jinsi ya kupiga vyema ala hiyo ambayo baadaye
ikamfanya aitwe Sorcerer of Guitar
(yaani Mchawi wa Gitaa).
Mwaka
1950, akiwa ndiyo kwanza ametimiza miaka 12, Franco alianza kutengeneza jina
wakati akiwa na bendi ya Watam iliyokuwa ikiongozwa na Paul Dewayon. Uwezo wake
wa kulikung’uta gitaa ulikonga nyoyo za mashabiki wengi ambao walistaajabia
umahiri wake wakati umri ukiwa unamsuta.
Miaka
mitatu baadaye Franco alirekodi wimbo wake wa kwanza uliokwenda kwa jina la Bolingo na Ngai na Beatrice (Mpenzi
wangu Beatrice). Baada ya kukubalika kuwa mmoja wa wana bendi ya Loningisa
Studio, kiongozi wa bendi hiyo Henri Bowane alitoa nadhiri kwamba angeishi na
Franco katika maisha yake yote yaliyosalia.
Chini
ya Henri Bowane, Franco akawa mpiga gita la solo ambapo alikuwa akipiga staili
ya Sebene na akaanza kutunga na
kuimba yeye mwenyewe kwa staili za rumba, za Kiafrika na hata za Kilatini.
Mnamo
Juni 1956 pamoja na kwamba alikuwa akipewa kazi nyingi katika studio, Franco akaamua
kuunda bendi akiwa na Jean Serge Essous na De La Lune ambao pia walikuwa
wakiimba pale Loningisa Studio. Bendi hii iliyokuwa ikifadhiliwa na
mfanyabiashara Omar Kashama wakaipa jina la OK Jazz ambapo ilikuwa ikipigia
katika Baa ya OK iliyokuwa ikimilikiwa na mfanyabiashara huyo.
Hapa
ndipo kwenye mkanganyiko kuhusu neno OK. Kiasili lilikuwa ni kifupisho cha Omar
Kashama, mfadhili wa bendi, lakini baadaye ikajipambanua na herufi hizo zikimaanisha
Orchestra Kinois.
Essous alikuwa
na kipaji cha upulizaji wa ala kuanzia clarinet hadi saxophone. Wanamuziki
wengine waanzilishi walikuwa mpiga bassAugustin Moniania Roitelet, mpiga drums La
Monta LiBerlin na Saturnin Pandy, mpiga gitaa Nicolas Bosuma Bakili Dessoin na
mwimbaji Philippe Lando Rossignol pamoja na Vicky Longomba.
Bendi
hiyo, ikiwa imesheheni vijana wenye vipaji na usongo wa kufanya vizuri kwenye
muziki, ghafla ikaanza kuziteka hisia za mashabiki wa muziki nchini Congo.
Ilikuwa wazi kwamba hawa jamaa hawakuwa wamedhamiria kupiga muziki wa
kujiburudisha, bali kupata mafanikio zaidi wakipiga rhumba lenye kasi siyo kama
lile la Africa Jazz ya Joseph Kabaselle ‘Le Grand Kalle’. Kila siku walipiga
muziki kwenye studio iliyokuwa ikimilikiwa na Mgiriki mmoja na mara chache
wakawa wanatumbuiza kwenye sherehe kama harusi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni