Jumanne, 19 Desemba 2017

Ramaphosa kuwa kiongozi mpya wa chama tawala cha ANC nchini A-Kusini

Cyril Ramaphosa amechaguliwa kuwa kiongozi mpya wa chama tawala cha ANC nchini A-Kusini .


Cyril Ramaphosa amechaguliwa kuwa kiongozi mpya wa chama tawala cha ANC nchini A-Kusini .
Ramposa ambaye alikuwa makamu wa rais wa chama hicho aliweza kumshinda mpinzani wake Nkosazana Dlamini-Zuma, ambaye ni waziri wa zamani na alikuwa mke wa rais Zuma kwa kura 2440 kwa 2161.
Kwa sasa Ramaphosa ameoneka kuwepo kwenye nafasi kubwa ya kuwa rais katika uchaguzi wa mwaka 2019.
Hata hivyo Cyril Ramposa amekuwa kiongozi wakati ambao Afrika kusini inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinafanya mambo hayendi sawa katika taifa hilo lenye uchumi mkubwa barani Afrika .

 Cyril Ramposa alizaliwa tarehe 17 mwezi novemba mwaka 1952 mjini Soweto, ndio mwanasiasa tajiri zaidi Afrika Kusini ,utajiri wake unakisiwa kuwa ni dola milioni 450.Tangu ujana wake Ramposa alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasiasa shupavu na hiyo ndio ilimfanya kujiunga na uongozi wa chama cha wafanyakazi .



afrikaafrika


Badaye Ramaphosa alishangaza wengi alipojiuzulu kutoka kwenye siasa na kushughulika zaidi katika biashara zake,lakini mwaka 2012 alishawishika tena na kurudi kwenye siasa na kuwa na ilipofika mwaka 2014,alipanda zaidi na kuwa makamu wa rais Zuma.
Na wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kurudi kwake Ramaphosa kwenye chama cha ANC kulirudisha imani ya wananchi wengi licha ya kuwa chama hicho kilikuwa kinakabiliwa na kashfa nyingi za kisiasa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni