Jumanne, 12 Desemba 2017

Guterres kuzungumza na Rais Magufuli wa Tanzania



Kufuatia mauaji ya walinda amani 14 wa Tanzania huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC siku ya Alhamisi na wengine zaidi ya 44 kujeruhiwa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres muda wowote sasa atazungumza kwa njia ya simu na Rais John Magufuli wa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki nchini Tanzania, Balozi Augustine Mahiga amesema hayo akihojiwa na Idhaa hii kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam.





 alikadhalika amesema Mkuu wa operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa Jean-Pierre Lacroix pamoja na msaidizi wake Atul Khare wanatarajiwa kuwasili nchini Tanzania muda wowote.
Jijini Dar es salaam, nchini Tanzania wakati wa mapokezi ya miili ya walinda amani wa Tanzania waliouawa huko Semuliki, jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC. (Picha:Mshirika/Issa Michuzi)
Wakati huo huo, ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, Alhamisi hii utakuwa na tukio maalum la kumbukizi ya mauaji ya walinda amani hao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni