Ijumaa, 15 Desemba 2017

BREAKING: Mbunge Upendo Peneza (CHADEMA) anazungumza na wanahabari



 Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema) anazungumza na vyombo vya habari.


Mbunge wa Chadema, Upendo Peneza amezua gumzo kwenye mitandao ya kijamii baada ya mbunge huyo kuitisha mkutano na waandishi wa habari bila kueleza atakachozungumza na wengi wameanza kutabiri huenda na yeye akatangaza maamuzi magumu ya kukihama chama hicho.

Peneza mbunge kutoka Mkoa wa Geita ameitisha mkutano huo kipindi ambacho kumekuwa na vuguvugu la wabunge kukikimbia chama hicho na kujiunga na CCM.

Mkutano huo umeitisha ikiwa ni siku moja kupita tangu mbunge wa Siha wa Chadema, Dk Godwin Mollel alipotangaza kuhamia CCM akiunga jitihada za Rais John Magufuli.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni