
Rais mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. Jakaya Kikwete amekubali shamba lake la mifugo lililopo kijijini kwake Msoga Bagamoyo litumike kama shamba darasa.
Mh. Jakaya Kikwete amekubali ombi hilo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha
Kilimo (SUA) kilichopo mkoani Morogoro, baada ya kutembelea chuoni hapo
akiwa na wataalamu wake wa mifugo kwa lengo la kujifunza mambo
mbalimbali kuhusu kilimo na mifugo.
Mh. Jakaya Kikwete amekubali ombi hilo kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine cha
Kilimo (SUA) kilichopo mkoani Morogoro, baada ya kutembelea chuoni hapo
akiwa na wataalamu wake wa mifugo kwa lengo la kujifunza mambo
mbalimbali kuhusu kilimo na mifugo.
Uongozi wa SUA ukatumia nfasi hiyo kuwasilisha ombi lao kwa Mh. Kikwete
ambaye alikubali na rasmi kuingia makubaliano ya pamoja ili kulitumia
shamba lake la mifugo kama shamba darasa la kutolea elimu ya vitendo kwa
wanafunzi wao, wataalamu wa mifugo na wafugaji.
Aidha Rais Mstaafu ameeleza kulizishwa na mafunzo aliyoyapata chuoni
hapo na kutoa ahadi ya kuendelea kushirikiana na chuo hicho kwa lengo la
kuleta mabadiliko ya kisayansi ya sekta ya ufugaji iweze kumletea tija
mfugaji.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni