
Mvua ya inayoendelea kunyesha kwa siku mbili mfululizo katika jiji la
Dar es salaam, imesababisha mafuriko makubwa katika maeneo mbalimbali
Jijini humo, ikiwemo eneo la Jangwani ambapo maji hayo yamefunga
mawasiliano ya barabara ya Morogoro, Hakuna gari inayokwenda wala kurudi
mjini.
Mpaka sasa umeripotiwa kuokotwa katika mto kenge uliopo Tabata jijini humo, mwili wa mtu mmoja mwenye jinsia ya kiume.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema
amefika katika eneo hilo nakuwataka wananchi kuondoka katika maeneo hayo
kwasasa kwakuwa maji yanaendelea kuongezeka.



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni