Alhamisi, 26 Oktoba 2017

MAFURIKO DAR, Nyumba zafunikwa na maji




Mvua ya inayoendelea kunyesha kwa siku mbili mfululizo katika jiji la Dar es salaam, imesababisha mafuriko makubwa katika maeneo mbalimbali Jijini humo, ikiwemo eneo la Jangwani ambapo maji hayo yamefunga mawasiliano ya barabara ya Morogoro, Hakuna gari inayokwenda wala kurudi mjini.
Mpaka sasa umeripotiwa kuokotwa katika mto kenge uliopo Tabata jijini humo, mwili wa mtu mmoja mwenye jinsia ya kiume.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema amefika katika eneo hilo nakuwataka wananchi kuondoka katika maeneo hayo kwasasa kwakuwa maji yanaendelea kuongezeka.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni